HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Thursday 8 August 2024

RUTO ALITUMIA NJAA YA RAILA

 


RAIS William Ruto alitumia azma ya uenyekiti wa Tume ya Muungano wa Afrika (AUC) ya kiongozi wa Azimio la Umoja, Bw Raila Odinga, kama mtego hadi akakubali chama chake kushirikiana na serikali kisiasa.

Wachambuzi wa siasa wanasema kwamba Bw Raila hakufaulu kujinasua kwenye mtego wa Rais Ruto kwa kuwa anataka kuungwa mkono na serikali katika azma yake ya kugombea wadhifa huo wa Bara.

Kiongozi wa chama cha Narc Kenya, Bi Martha Karua anasema Bw Odinga aliangukia mtego na hila za kisiasa alizowekewa kijanja na Rais Ruto.

Kulingana na Bi Karua, Bw Raila alijiondoa katika siasa za upinzani ili kuzingatia kampeni yake ya uenyekiti wa AUC ambayo anahitaji kuungwa mkono na serikali ya Kenya.

“Raila alijiondoa katika siasa za upinzani ili kufanya kampeni zake za kuwania kiti cha AU ambacho anahitaji Kenya Kwanza ndipo akipate.

Ni lazima apendekezwe na serikali ya Kenya na nadhani hapa ndipo mtego ulipomnasa na unaweza kuona wakati wa kuingia serikalini ni ule ambao stakabadhi zake ziliwasilishwa rasmi,” Bi Karua alisema kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio hivi majuzi.

Kiongozi wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka, amejitangaza kuwa kiongozi wa muungano wa upinzani wa Azimio la Umoja-One Kenya huku Bw Raila akiendelea na kampeni zake za kugombea wadhifa wa Bara.

Bi Karua anasema kuwa Bw Raila hana budi kuunga serikali iwapo anataka azma yake ya kiti cha AU ifaulu.

Hapa, kulingana na Bi Karua, ndipo mtego ulipotegwa na Rais Ruto.

Katika tukio ambalo Rais Ruto alitaja kama serikali jumuishi, kiongozi huyo wa Azimio alitoa baadhi ya viongozi wa ODM kuteuliwa katika Baraza la Mawaziri la serikali ya Kenya Kwanza.

Bw Ruto aliteua manaibu viongozi wa ODM, Ali Hassan Joho, Wycliffe Oparanya, Kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa Opiyo Wandayi na mwenyekiti wa kitaifa wa chama hicho John Mbadi.

Bi Karua aliondoa chama chake katika muungano wa Azimio kufuatia hatua ya ODM kujiunga na serikali. Katika hafla zaidi ya moja, Bw Raila alikanusha makubaliano ya aina yoyote na Rais Ruto.

Hata hivyo, mnamo Jumatatu, waziri huyo mkuu wa zamani alipokuwa akizungumza katika Soko la Toi, Nairobi, alidai kuwa Rais Ruto aliomba msaada kutoka kwake ili kukomesha vuguvugu la Gen-Z ambalo lilikuwa likitishia kupindua serikali yake.

“Uliona wamelemewa na kazi, wakawafuta kazi waziri, wakaja kwetu wakiomba watu. Walikuja wakipiga magoti wakiomba tuwachangie baadhi ya watu,” Raila alifichua.

Kulingana na mchambuzi wa siasa, Dkt Isaac Gichuki, Bw Raila alijipata katika mtego asioweza kujinasua kwa kutaka serikali iidhinishe azma yake ya kugombea uenyekiti wa AUC.

“Kile ambacho Bw Raila na Ruto hawawezi kukiri ni kwamba kila mmoja alihitaji mwingine. Raila alihitaji Ruto zaidi katika azma yake ya AUC naye Ruto alihitaji Raila amsaidie kuokoa serikali yake iliyotishiwa na maandamano ya vijana,” akasema.

Wednesday 7 August 2024

MAGAVANA CHINI YA MWENYEKITI WAO WATISHIA KUZIMA NDOTO YA SHIF IWAPO MALIPO YA NHIF HAYATATIMIZWA

 

Ann Waiguru akiongea na wanahabari

MAGAVANA wanaitaka Wizara ya Afya kupatia kipaumbele malipo ya Sh8 bilioni ambazo Hazina ya Kitaifa ya Bima ya Kitaifa (NHIF) inadaiwa na hospitali za kaunti kabla ya kuhamia katika Hazina ya Afya ya Jamii (SHIF).

Miezi kadhaa baada ya hospitali za kibinafsi kote nchini kuondoa huduma zao kwa Wakenya walio na kadi za NHIF kutokana na deni lingine, ni hospitali za umma za kaunti pekee zinazokubali kadi za NHIF na kuwalazimu Wakenya kutoka jamii maskini kufurika katika hospitali za umma kusaka huduma za afya.

Magavana wameonya kuchelewesha kumaliza kulipa deni hilo kutawasababishia mateso zaidi Wakenya wenye mapato ya chini wanaotegemea huduma hizo.

Kaunti za Nairobi na Nakuru ni miongoni mwa zinazodai NHIF kiasi kikubwa cha pesa huku Nairobi ikidai kiasi kisichopungua Sh2.1 bilioni na Nakuru Sh540 milioni kutoka kwa NHIF na Linda Mama.

“Tunapohamia SHIF, hatutaki kuona hali ambapo Sh8 bilioni zinageuka kuwa malimbikizi ya deni ambalo halijalipwa kwa vituo vya afya. Tunataka NHIF ilipe vituo ambavyo madeni yake yangali hayajalipwa. Ni kwa namna hiyo tu tutaweza kuhamia SHIF bila deni lolote linalodaiwa na vituo vya kaunti,” Mwenyekiti wa Kamati ya Afya katika Baraza la Magavana, Gavana Muthomi Njuki alisema Jumanne.

Gavana wa Nakuru, Bi Susan Kihika, alielezea wasiwasi wake, akisema Nakuru pekee inadai NHIF na mpango wa Linda Mama kitita cha Sh540 milioni.

“Hali ya kukosa kulipa ni mzigo mzito mno kwa hospitali zetu na huenda hivi karibuni ikalemaza oparesheni. Tunahimiza Wizara ya Afya kupatia kipaumbele deni kwa sababu hospitali zetu tayari zimeathirika vibaya na kucheleweshewa malipo. Jijini Nakuru, kwa mfano, tunaona bidhaa zinazozidi kuwasilishwa lakini tunabeba mzigo kwa sababu hatupati malipo,” alisema Gavana Kihika.

Wizara ya Afya (MoH) na Baraza la Magavana (CoG) linaloongozwa na Gavana wa Kirinyaga, Bi Anne Waiguru, hapo mbeleni limekutana kujadili masuala yanayohusu madeni huku mchakato wa kuhamia SHIF ukiendelea.

Mikutano hiyo iliangazia masuala muhimu ambayo ni pamoja na madeni.

MoH na serikali za kaunti zimeafikiana vilevile kuendesha kampeni ya umma kuhusu usajili wa wanachama wanaojiunga na SHIF.

Pande hizo mbili zitaendelea kushirikiana ili kuhakikisha utekelezaji bora wa Mpango wa Afya kwa Wote (UHC).

Waliafikiana vilevile kuwa MoH itatumia mfumo na data inayotumika kwa sasa katika NHIF iliyovunjiliwa mbali, kabla ya kuzindua SHIF.

MAHAKAMA YAMWAGILIA MAJI BARIDI UWEZEKANO WA DCI KUWAKAMATA WANDANI WA GACHAGUA WANAOSHUKIWA KUPANGA MAANDAMANO YA GEN Z

 

Naibu Rais Gachagua kwenye picha    

MAHAKAMA Kuu imeamuru polisi wasiwatie nguvuni wabunge wawili wanaodaiwa kufadhili maandamano ya vijana yaliyopelekea watu zaidi ya 60 kuuawa na zaidi ya watu 600 kujeruhiwa.

Jaji Enock Chacha Mwita aliwaamuru Inspekta Jenerali wa Polisi na Mkurugenzi wa Idara ya Uchunguzi wa Jinai (DCI) Mohamed Amin wasiwakamate Wabunge James Mwangi Gakuya (Embakasi North) na Benjamin Gathiru almaarufu Mejja Donk (Embakasi Central).

“Baada ya kusikiza mawasilisho ya mawakili Danstan Omari na Shadrack Wambui pamoja na kuchambua ushahidi ulioambatishwa na ombi la Gakuya na Gathiri, ni bayana haki zao zitakandamizwa na wako na ombi lililo na mashiko kisheria,” alisema Jaji Mwita.

Jaji Mwita alifahamishwa na mawakili Bw Omari na Bw Wambui, kwamba wanasiasa hao wanalengwa na haki zao kukandamizwa na polisi kwa vile ni wandani wa Naibu Rais Rigathi Gachagua.

“Hakuna ukweli wowote wawili hawa wanafadhili maandamano ya Gen Z. Kila mtu amepewa idhini ya kuandamana kwa mujibu wa Kifungu nambari 37 cha Katiba kuelezea kutoridhika kwao na uongozi mbaya wa Serikali,” Mabw Omari na Wambui walimweleza Jaji Mwita.

Mawakili hao walimueleza Jaji Mwita kwamba maafisa kutoka kitengo cha DCI na kile cha ujasusi (NIS), waliwatia nguvuni wabunge na kuwanyang’anya simu zao za rununu kwa madai walikuwa wakipanga njama za maandamano na kufadhili uhuni wakati wa maandamano ya Gen Z.

“Inspekta Philip Sang alipata agizo kutoka kwa Hakimu Mkuu wa mahakama ya Kiambu kuchunguza mawasiliano ya simu ya Mabw Gakuya na Gathiru kubaini ukweli wa habari za kijasusi kwamba wawili hao ndio wanaofadhili uhuni wakati wa maandamano ya Gen Z,” Bw Omari alimweleza Jaji Mwita.

Jaji Mwita aliwaagiza mawakili hao wawakabidhi Waziri wa Usalama wa Ndani, IG, DCI na Mwanasheria mkuu nakala za kesi hiyo katika muda wa siku 7 kuanzia Agosti 6, 2024 ndipo wawasilishe majibu mahakamani dhidi ya madai ya kuhujumu haki za Mabw Gakuya na Gathiru.

Tuesday 6 August 2024

WALZ KUWA TEGEMEO LA HARRIS KATIKA KURA ZA MASHAMBANI ANYOTEGEMEA TRUMP.

 


MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.

Waltz anasifiwa kama mwenye kipawa cha usemi na mtetezi sugu wa sera endelevu nchini Amerika.

Anatarajiwa kumsaidia Harris kuvutia kura katika maeneo ya mashambani na kura za Waamerika weupe.

Hata hivyo, maafisa wa kikosi cha kampeni za makamu huyo wa rais walidinda kutoa maelezo zaidi kuhusu suala hilo.

Walz, 60, ambaye ni shujaa wa zamani wa Jeshi la Kitaifa la Amerika na mwalimu, alichaguliwa kama Mbunge katika Bunge la Wawakilishi mnamo 2006 ambako alihudumu kwa miaka 12 kabla ya kuchaguliwa Gavana wa Jimbo la Minnesota mnamo 2018.

Akihudumu kama Gavana, Walz alitetea ajenda endelevu zilizojumuisha utoaji wa lishe shule bila kulipiwa, malengo ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, punguzo la ushuru kwa watu wa tabaka la kati na kuanzishwa kwa sera za wafanyakazi kulipwa wakiwa likizoni katika jimbo la Minnesota.

Walz ametetea haki za uzazi za wanawake

Aidha, kwa muda mrefu, Walz ametetea haki za uzazi za wanawake, masilahi ya wadau katika sekta ya kilimo na kuunga mkono haki kuhusu umiliki wa bunduki na raia.

Aliendeleza utetezi huo alipohudumu kama mwakilishi wa eneo la mashambani katika Bunge la Wawakilishi.

Harris, ambaye ni binti ya wahamiaji kutoka Jamaica na India, anatarajia kuwa mwanasiasa kutoka jimbo ambalo wapiga kura wake wengine huunga mkono chama cha Republican katika chaguzi za urais, atamfaa zaidi.

Jimbo hilo la Minnesota pia linapakana na majimbo mawili ya Wisconsin na Michigan, ambayo hushindaniwa kwa ukaribu na chama hicho na kile cha Republican.

Majimbo kama hayo huonekana kama muhimu katika kuamua mshindi katika chaguzi za urais zilizopita sawa na uchaguzi ujao.

Walz anaonekana na wengi kama mwenye ujuzi wa kuwavutia wapiga kura weupe na wale wa maeneo ya mashambani ambao katika miaka michache iliyopita wamemuunga mkono mgombeaji wa chama cha Republican Donald Trump.

Harris alimteua Walz badala ya gavana wa Pennsylvania Josh Shapiro, ambaye alitarajiwa kumpa ushindi katika jimbo hilo muhimu.

Makamu huyo wa Rais aliteuliwa mgombeaji urais wa Chama cha Democrat baada ya bosi wake, Rais Joe Biden kujiondoa katika kinyang’anyiro cha kutafuta muhula wa pili Ikuluni mwezi jana.

Tangu wakati huo, amechangiwa fedha nyingi za kufadhili na kutoa mwelekeo mpya katika kampeni dhidi ya Trump.

Jumanne jioni, Harris alitarajiwa kujitokeza na mgombea mwenza wake katika mkutano wa kampeni katika mji wa Philadelphia.

Inatarajiwa kuwa tajriba pana ya Walz jeshini na ufanisi wake kama kocha wa kandanda katika shule ya upili itavutia wapiga kura ambao hawataki Trump ahudumu kwa muhula wa pili katika Ikulu ya White House.

Aidha, imeripotiwa kuwa Gavana huyo wa Minnesota alikuwa akiungwa mkono na aliyekuwa Spika wa Bunge Nancy Pelosi, aliyechangia pakubwa katika kumshawishi Rais Biden, 81, ajiondoe kinyang’anyironi.

Harris na Walz sasa watakabana koo na Trump na mgombea mwenza wake JD Vance, ambaye pia ni mwanajeshi wa zamani, katika uchaguzi wa Novemba.

https://technofreak-cooldude.blogspot.com/2009/07/how-to-add-moving-text-to-blog-or.html

 https://technofreak-cooldude.blogspot.com/2009/07/how-to-add-moving-text-to-blog-or.html

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027

 


  1. <div class="scrollbox">

NAIBU Rais Rigathi Gachagua sasa anasema kuwa yuko tayari kumkumbatia kisiasa Kinara wa Upinzani Raila Odinga na atamfikia ili washirikiane naye katika uchaguzi wa 2027.
  1. </div>

Kauli hiyo ya Bw Gachagua inakuja wakati ambapo Bw Odinga ameanza kushirikiana kisiasa na Rais William Ruto na hata wandani wake wakateuliwa serikalini.

Naibu Rais alisema kuwa mwanasiasa huyo wa upinzani si adui wa Mlima Kenya jinsi ambavyo imekuwa ikifasiriwa huku akidai alipotoshwa ndiposa amekuwa akimpinga katika siasa za nchi.

“Mimi nimekuwa nikibeba ile dhana kwamba Bw Odinga sio mtu wa kuaminiwa au wa kushirikiana naye kisiasa. Ndiyo sababu sisi katika eneo la Mlima tumekuwa tukijitenga naye,” akasema Bw Gachagua.

Alikuwa akizungumza mnamo Jumapili usiku, Agosti 4, 2024 wakati alipokuwa akihojiwa na runinga ya Inooro ambayo inapeperusha matangazo yake kwa lugha ya Kikuyu.

“Kwa sasa nataka ieleweke kwamba Bw Odinga ni mmoja wa marafiki wetu ambao hata tunaweza kushirikiana naye kisiasa siku zijazo. Tumemkumbatia kama jamii kwa sababu Rais Ruto amemleta ndani ya serikali na tutachapa kazi pamoja na hatimaye muda ukifika, tuongee kuhusu ndoa kwa siku zijazo za miereka ya kisiasa,” akaongeza.

Bw Gachagua amekuwa hasimu mkubwa wa kisiasa wa waziri huyo mkuu wa zamani na alikuwa kati ya wanasiasa waliomtahadharisha Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta dhidi ya kufanya kazi na kiongozi huyo wa ODM.

Kile ambacho kimeunganisha Naibu Rais na Bw Odinga kimtazamo ni wote kuunga mkono ugavi wa mapato kwa kutegemea idadi ya watu wala si ukubwa wa eneo.

Wito huo umemweka Bw Gachagua pabaya na baadhi ya wanasiasa katika kambi ya Kenya Kwanza, wengi wakimwona kama anayepigania tu maslahi ya wakazi wa Mlima Kenya.

“Tumefunguka macho sasa na nitaongoza harakati za kumpendekeza Bw Odinga kama mshirika wetu wa dhati Mlimani kama ilivyokuwa katika kinyang’anyiro cha 2022 akisaidiana na Bw Kenyatta,” akasema.

Wakati wa mahojiano hayo, Naibu Rais alirejelea kauli yake kuwa alikuwa amemwekea Bw Odinga mtego kwenye ikulu.

Alisema ni Rais Ruto ndiye alimshauri ayatoe matamshi hayo na kwa kweli aliwajibika kwa kuwa kiongozi wa nchi na Bw Odinga walikutana Uganda kwa Rais Yoweri Museveni.

Alifunguka na kusema kuwa hatua ya Bw Odinga kuunga kauli yake kuhusu mgao wa rasilimali ni ishara tosha kuwa waziri huyo mkuu wa zamani anafahamu masuala ya uongozi wa nchi hii.

“”Nilikemewa sana hata na viongozi wenzangu wa Mlima Kenya. Lakini nilishangaa kumsikia Bw Odinga akiniunga mkono hadharani,

“Bibi yangu aliniambia kwamba roho imemfunulia kwamba Bw Odinga ni yule malaika wa nia njema ambaye kumtambua ni lazima kuwe na ufunuo. Ufunuo huo ndio hatujawahi kuwa nao kama watu wa Mlima na ndipo tukamchukia,” akasema.

Sifa hizi kochokocho ambazo Bw Gachagua amemiminia Raila zinakuja wakati ambapo kumekuwa na madai kuwa naibu rais anapanga kuanzisha ndoa ya kisiasa na Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka.

Licha ya kukita sana siasa zake eneo la Mlima Kenya, wakati wa mahojiano hayo, Bw Gachagua alifunguka na kusema yupo tayari pia kuanzisha ushirikiano na Gavana wa Trans Nzoia George Natembeya na Kiongozi wa DAP Kenya Eugene Wamalwa.

Kumkumbatia Bw Odinga kuna kuja wakati ambapo washirika wa mbunge huyo wa zamani wa Lang’ata nao wameteuliwa ndani ya serikali kutokana na ukuruba wake na Rais Ruto.

Kando na kutunukiwa mawaziri watano, mwanasheria mkuu mteule Dorcas Oduor pia anatoka Nyanza, ngome ya kisiasa ya Raila.

Pia kuna mabadiliko yanayotarajiwa ya makatibu wanaodumu serikalini ambapo inadaiwa kinara huyo wa upinzani atavuna vinono.

Bw Gachagua mwenyewe amekuwa akilalamika kuwa wandani wake wanahangaishwa na makachero wa Idara ya Upelelezi Nchini (DCI) pamoja na maafisa kutoka Shirika la Kijasusi (NIS).

Kati ya wandani wake aliosema wamekuwa wakifuatiliwa, kuhangaishwa na mawasiliano yao kurekodiwa ni Mbunge wa Embakasi Kaskazini James Gakuya na mwenzake wa Embakasi ya Kati Benjamin Gathiru maarufu kama Meja Donk.

Wakati wa mahojiano hayo, Naibu Rais alionekana kuwa na tofauti kubwa na bosi wake akisema kuwa hata hakuhusishwa au kushauriwa wakati ambapo katibu mkuu wa chama cha UDA, Bw Cleophas Malala aling’atuliwa mamlakani wiki jana.

LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!

 


GAVANA wa Kaunti ya Bungoma, Kenneth Lusaka, Jumatatu, Agosti 5, 2024 alisimamisha kwa muda kikao cha Seneti akitaka Seneta aliyemdhalilisha kwa kumtusi kumuomba msamaha.

Bosi huyo wa gatuzi la Bungoma alifika mbele ya Kamati ya Seneti kuhusu Ugatuzi ambapo alitakiwa kujibu maswali kuhusu akaunti za Benki ya Commercial (KCB) zinazoendeshwa na kaunti yake.

Hata hivyo, kabla ya kikao hicho kuanza, Gavana Lusaka alieleza Kamati hiyo kwamba Seneta wa Kisii, Richard Onyonka, alimkosea heshima kwa kumwita ‘mpumbavu” na kumtaka aombe radhi.

Haya yalijiri kufuatia ripoti kuwa usimamizi wa kaunti ya Bungoma ulitumia kitita cha Sh25 milioni kwa urembeshaji, ikiwemo kununua maua wakati wa Sikukuu ya Madaraka, mwaka huu, 2024.

Kulingana na Gavana Lusaka, madai hayo hayana msingi wowote kumruhusu Seneta wa Kisii kumshambulia kwa maneno mazito.

“Mialiko hutokana na ripoti ya mdhibiti wa bajeti, ndiposa tuko hapa. Lakini wakati ambapo suala hata halijashughulikiwa na kamati yoyote, mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, mdhibiti bajeti wala EACC, ni uvumi mitaani. Kisha tunalitumia kuunda taswira fulani si haki kabisa ukijua kuwa nitafika hapa,” alisema Gavana Lusaka.

“Mimi ni binadamu na nilihisi nimedhalilishwa kwa kuitwa mpumbavu. Nataka Seneta aombe radhi kwa matamshi hayo.”

Akijitetea, Seneta Onyonka alifafanua kwamba matamshi yake yalitokana na ghadhabu kuhusu ubadhirifu wa fedha uliokithiri Kaunti ya Bungoma akisema hakulenga nafsi ya Gavana.

“Gavana Lusaka wewe ni mwanamme ninayeheshimu mno, hakuna shaka kuhusu hilo. Nilipoona ripoti kuwa Gavana wa Bungoma alinunua maua ya Sh25 milioni nilipandwa na mori. Haikuwa kukuhusu, kauli hiyo haikukulenga. Ikiwa kauli hiyo ilikukwaza ninaomba radhi kwa dhati,” alisema Seneta Onyonka.

“Lakini nitakwambia leo Gavana, nikija leo katika Kituo cha Afya Bungoma nilipokuwa tukiandamana na mwenyekiti, tulipopata wanawake wamelala sakafuni, nakwambia bado nitasema, ‘hawa ni wapumbavu wanaofanya kazi katika kituo kama hiki.’ Mahali tunapowachukulia watu wetu maskini kwa kiwango duni zaidi kuliko tunavyowatendea mbwa wetu.”

Alisema matamshi yake hayakumlenga Gavana Lusaka bali “mifumo mibovu ya taifa langu, Kenya ambapo unasimamia karibu bilioni moja za kufadhili huduma za matibabu na wanawake wote katika kituo hicho…”

“Ukija hapa, huji ili tukueleze jinsi tulivyo safi nawe una hatia. Ni mdahalo jinsi ulivyosema. Uhalisia ni kuwa tulikuwa Bungoma na watu walikuwa wamelala sakafuni tulipoingia. Ukweli ni ule ule ila matamshi, tukizingatia hadhi yako, ninataka kusema samahani kwamba nilikusawiri hivyo.”

Kamati hiyo inayoongozwa na Seneta wa Kaunti ya Wajir, Abass Mohamed, ilielezwa kuwa, Gavana Lusaka vilevile amenukuliwa akitoa matamshi ya kudhalilisha viongozi wengine wakiwemo maseneta.

“Natoka kaunti anayotoka Gavana. Juzi alisema ukiona kobe juu ya meza bila shaka kuna mtu aliyeiwekelea hapo. Lakini sitaichukulia binafsi kwa sababu hatimaye kobe yuko hapa. Tusichukulie mambo kwa kibinafsi,” alisema Seneta Onyonka.

Monday 5 August 2024

GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu wa Bangladesh, Sheikh Hasina Wazed amejiuzulu na kuondoka nchini humo, baada ya wiki kadhaa za maandamano yaliyoongozwa na wanafunzi na kupelekea machafuko makubwa nchini kote. Ripoti zinasema, bibi huyo mwenye umri wa miaka 76 alikimbia kwa helikopta Jumatatu hadi India, wakati maelfu ya waandamanaji wakivamia makazi yake katika mji mkuu wa Dhaka. Hilo limemaliza utawala wa Waziri Mkuu aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi nchini Bangladesh, kwa zaidi ya miaka 20 jumla. Anasifiwa kwa kusimamia maendeleo ya kiuchumi ya nchi hiyo ya Kusini mwa Asia, hata hivyo katika miaka ya hivi karibuni Bi Hasina ameshutumiwa kwa kugeuka kuwa kiongozi wa kiimla. Aliingiaje madarakani? Alizaliwa katika familia ya Kiislamu huko Bengal Mashariki mwaka 1947, Bi Hasina anatokea familia ya wanasiasa. Baba yake Sheikh Mujibur Rahman, 'Baba wa Taifa' la Bangladesh, alikuwa kiongozi mzalendo aliyeongoza uhuru wa nchi hiyo kutoka Pakistan mwaka 1971 na kuwa rais wa kwanza. Wakati huo, Bi Hasina alikuwa tayari anajuulikana kwa kuwa kiongozi wa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dhaka. Rahman aliuawa pamoja na watu wengi wa familia yake katika mapinduzi ya kijeshi mwaka 1975. Bi Hasina na dadake mdogo ndio pekee walionusurika kwani walikuwa safarini nje ya nchi wakati huo. Baada ya kuishi uhamishoni nchini India, Bi Hasina alirejea Bangladesh mwaka 1981 na kuwa kiongozi wa chama cha kisiasa cha babake, Awami League. Aliungana na vyama vingine vya kisiasa kufanya maandamano mitaani ya kuunga mkono demokrasia, wakati wa utawala wa kijeshi wa Jenerali Hussain Muhammed Ershad. Vuguvugu hilo lilimfanya Bi Hasina akawa mwanasiasa wa kitaifa haraka sana. Aliingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 1996. Alipata sifa kwa kutia saini mkataba wa kugawana maji na India na mapatano ya amani na waasi kusini-mashariki mwa nchi hiyo. Lakini wakati huo huo, serikali yake ilikosolewa kwa mikataba mingi ya kibiashara inayodaiwa kuwa ni mbovu na kwa kuwa mtiifu sana kwa India. Baadaye alishindwa na mshirika wake wa zamani aliyegeuka kuwa mpinzani, Bi Begum Khaleda Zia wa chama cha Bangladesh Nationalist Party (BNP), mwaka 2001. Wanawake wote wawili wametawala siasa za Bangladesh kwa zaidi ya miongo mitatu na wanajulikana kama "Begums wanaovutana." Begum ina maana ya mwanamke wa Kiislamu wa daraja la juu. Waangalizi wanasema ushindani wao mkali umesababisha mlipuko wa mabomu katika mabasi, kutoweka na mauaji ya kiholela ya mara kwa mara. Bi Hasina hatimaye alirejea mamlakani mwaka 2009 katika uchaguzi uliofanyika chini ya serikali ya mpito. Akiwa mwathirika wa kisiasa, amekamatwa mara kadhaa akiwa upinzani na vile vile majaribio kadhaa ya kumuua, likiwemo moja la mwaka 2004 ambalo liliharibu usikivu wake. Pia amenusurika juhudi za kumlazimisha Kwenda uhamishoni kwa kesi nyingi mahakamani zinazomshutumu kwa ufisadi. Mafanikio yake ni yapi? Bangladesh, taifa lenye Waislamu wengi, lilikuwa mojawapo ya mataifa maskini zaidi duniani, limepata mafanikio makubwa ya kiuchumi chini ya uongozi wake tangu 2009. Sasa ni moja wapo ya taifa lenye uchumi unaokua kwa kasi katika eneo hilo, hata kupita jirani yake mkubwa India. Pato la taifa kwa mtu mmoja limeongezeka mara tatu katika muongo uliopita na Benki ya Dunia inakadiria kuwa zaidi ya watu milioni 25 wameondokana na umaskini katika miaka 20 iliyopita. Sehemu kubwa ya ukuaji huu imechochewa na sekta ya nguo, ambayo inachangia idadi kubwa ya mauzo ya nje ya nchi na sekta hiyo imekuwa katika miongo ya hivi karibuni, ikisambaza nguo katika masoko ya Ulaya, Amerika Kaskazini na Asia. Serikali ya Bi Hasina imefanya miradi mikubwa ya miundombinu kwa kutumia fedha za nchi hiyo, mikopo na usaidizi wa maendeleo, ikiwa ni pamoja na daraja kubwa la Padma lililogharimu dola za kimarekani bilioni 2.9 huko Ganges.

AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA

WANAFUNZI 26, walimu watatu na mpishi mmoja wa shule ya Rockside Academy, Nairobi wanapokea matibabu katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Nakuru na Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Molo baada ya gari lao kuhusika katika ajali eneo la Sachangwan, Nakuru, Jumatatu, Agosti 5, 2024. Kwa mujibu wa Kamanda ya Polisi wa Kaunti Ndogo ya Molo Timon Odingo, basi hilo la shule lilikuwa likiwasafirisha wanafunzi kutoka Eldoret ambako walikuwa wameshiriki tamasha za muziki zinazoendelea. Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa saba za mchana baada ya lori kutoka nyuma kupoteza mwelekeo na kugonga basi hilo kutoka nyuma. Baadaye lori hilo liligonga magari mengine mawili ya kibinafsi hadi yakaanguka kwenye mtaro kando ya barabara. Watu 30 walipata majeraha katika ajali hiyo, japo waliokuwa kwenye magari ya kibinafsi hawakuathiriwa. Maafisa wa polisi walipowasili katika eneo la ajali wenyeji na wasamaria wema walikuwa tayari wamewaondoa waathiriwa. “Waliojeruhiwa wamekimbizwa hospitalini na sasa wanapokea matibabu. Kwa bahati nzuri hakuna aliyekufa. Maafisa wa polisi wametumwa hospitali kuendeleza uchunguzi,” Bw Odingo akasema.

Friday 19 July 2024

RAIS RUTO AKOSOLEWA KWENYE BARAZA LAKE JIPYA LA WATU 11 AKIWAHUSISHA WALIOFURUSHWA

Rais william ruto hatimaye ametangaza baraza la mawazi ambayo kwa sasa inakosolewa pakubwa na watu mbalimbali.je atayaweza Interior - Kithure Kindiki Health - Dr. Debra Mulongo Barasa Public Works - Alice Wahome Education - Julius Ogamba Defence - Aden Duale Agriculture - Dr. Andrew Karanja Environment - Soipan Tuya Water - Eric Muriithi Roads - Davis Chirchir ICT - Dr. Margaret Ndungu AG - Rebecca Miano

Wednesday 17 July 2024

KITUO CHA PEPEA RADIO SASA YASIKIKA VYEMA MTANDAONI

Sasa unawezasikiliza pepea radio inakuwa kivutio kikubwa kwenye mtandao kwa burudani tosha.bonyeza tu hii link hapa upate uhondo https://zeno.fm/radio/pepea-radio/ ama tafuta tu PEPEA RADIO kwenye google search

WANAHABARI WAPANGA MAANDAMANO TAREHE 24 JULAI

JUMATANO, Julai 24, 2024, itakuwa zamu ya wanahabari kujitokeza barabarani kote nchini kwa maandamano ya kupinga dhuluma wanazotendewa na polisi wakiwa kazini. Akitoa ilani kuhusu maandamano hayo, rais wa Chama cha Wahariri Nchini (KEG) Zubeida Kananu Jumatano alilaani visa vya wanahabari kushambuliwa na polisi wakiwa kazini akisema vinahujumu uhuru wao ambao unalindwa na katiba. Bi Kananu alitoa mifano ya visa vya hivi punde vya kupigwa risasi kwa ripota wa Shirika la Habari la Mediamax Catherine Wanjeri Kariuki na polisi wakikabiliana na waandamanaji mjini Nakuru na kutekwa nyara kwa mwanahabari mkongwe Macharia Gaitho na watu waliodaiwa kuwa maafisa wa polisi. “Kwa hivyo, tumekubaliana kwamba mnamo Jumatano wiki ijayo wanahabari watafanya maandamano kulaani vitendo kama hivi vya kikatili wanavyotendewa na polisi wanapotekeleza majukumu yao,” akasema alipoandamana na Bw Gaitho kuandikisha taarifa katika Afisi za Mamlaka ya Kuchunguza Utendakazi wa Polisi (IPOA). Hii ni kufuatia kisa cha Jumatano asubuhi ambapo mwanahabari huyo alitekwa mara na watu waliodai kuwa wao ni maafisa wa upelelezi kutoka Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI). Bw Gaitho alitendewa unyama huo katika Kituo cha Polisi cha Karen alikokimbilia baada ya kubaini kuwa alikuwa akiandamwa na maafisa hao waliokuwa kwenye gari la kibinafsi. Hata hivyo, baadaye DCI ilitoa taarifa ikidai maafisa wake walimkamata Bw Gaitho kimakosa kwani walikuwa wakimlenga mwanablogu Francis Gaitho. Bi Kananu alisema kuwa maandamano ya wanahabari yatakuwa ya amani na washiriki hawajihami kwa vitu vya kutishia amani. “Hatutajihami kwa mawe wala marungu, bali tutabeba kamera zetu, vijitabu na kalamu miongoni mwa vyombo vingine vya kazi. Sharti ulimwengu mzima ujue maovu yanayotendewa wanahabari nchini Kenya,” Bi Kananu akasema, akisisitiza. Katibu Mkuu wa Muungano wa Wanahabari Nchini (KUJ) Eric Oduor amethibitisha mipango ya maandamano hayo na kuwataka wanahabari wote nchini kushiriki. “Tutamjulisha rasmi Kaimu Inspekta Jenerali Douglas Kanja kuhusu nia yetu ya wanachama wetu kufanya maandamano kote nchini Jumatano wiki ijayo kupinga mwenendo wa polisi kushambulia wanachama wetu wakiwa kazini,” Bw Odour akaambia umma kwa njia ya simu.

SIMANZI KENYA JAJI OGEMBO AAGA DUNIA

Marehemu Jaji Daniel Ogembo, alipatikana Jumatano, Julai 17, 2024 akiwa ameaga dunia katika makazi yake rasmi mjini Siaya. Alitarajiwa kuongoza kikao asubuhi katika majengo ya Mahakama Kuu ya Siaya lakini akakosa kujitokeza hali iliyoibua shaka. Jaji Ogembo amehudumu kwa miaka miwili katika Mahakama Kuu ya Siaya alipokuwa jaji mkazi. Kamanda wa Polisi, Kaunti ya Siaya, Cleti Kimaiyo, alithibitisha kifo chake na kusema polisi na Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI) imeanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo. “Tutawafahamisha kuhusu matokeo, bado tunachunguza kiini cha kifo chake,” alisema mkuu wa polisi kaunti hiyo. Kulingana na afisa mmoja wa mahakama aliyechelea kutajwa kwa sababu ya uzito wa suala hilo, Jaji Ogembo alipatikana akiwa mfu asubuhi baada ya kukosa kujibu dereva wake alipokwenda kumchukua nyumbani kwake. “Dereva alimpeleka nyumbani Jumanne jioni lakini aliporejea asubuhi, jaji hakujibu hali iliyofanya dereva kuripoti kwa maafisa katika korti ya Siaya,” alisema afisa huyo wa ngazi ya juu. Kifo cha Jaji Ogembo kililemaza vikao vya korti huku wafanyakazi wakikumbwa na mshtuko kufuatia habari hizo. Kifo cha Jaji Ogembo kimetokea hata kabla ya wiki kuisha baada ya Jaji David Majanja kufariki dunia. Mwezi uliopita, Hakimu Mkuu wa Korti ya Makadara, Monicah Kivuti, aliuawa kwa kupigwa risasi na afisa mkuu wa polisi kutoka kituo cha Londiani.

Friday 30 June 2023

PEPEA RADIO NOW ONLINE

first started like ajoke but finally the dream has become true.A radio owned by TRANSMEDIA AFRICA LTD. Is set to be launched offgicially soon as it has already started airing its programmes.Peter Mukabi the owner of the statio reteriated that he consider mostly creativ mind.He told our newsdesk the radio stion wilat large cover news,east africa music and other related things.Peter Mukabi is one of the longest serving radio journalist in kenya. Sources indicates that most people across the world now tune into the stion.Mukabi revealed to us that he will be streaming alsso church events so that to reach deaper audiency.Talented youths are also encouraged to send application and proposalPeter Mukabi is the CEO of the statio

Friday 10 February 2023

BECKY AMWOGAH GOSPEL QUEEN FROM BUNGOMA

BECKY AMWOGAH

Brought up from a humble background,Becky Amwogah is one of the fasted growing gospel artist in kenya.Becky who started singing few years ago came to limelight after attending events and perform publicly.

According to our source Becky who comesfrom kakamega county and lives in bungoma is set to release her new song soon titled MAISHA YANGU which represents those who are discouraged and are looking upon the lord for their hopes.


Becky one of the living testimony who are ever fresh with full of ideas making the industry juicy 

Sunday 5 February 2023

AMANI NDIO NJIA TU ASEMA PAPA FRANCIS

 JUBA, SUDAN KUSINI

PAPA FRANCIS

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni Papa Francis ametoa wito kwa viongozi wa Sudan Kusini kuweka “mwanzo mpya” wa amani nchini humo.

Akiongea Ijumaa alipoanza ziara ya siku tatu katika nchi hiyo iliyozongwa na vita Papa huyo alionya kwamba historia itawahukumu vibaya viongozi hao kwa vitendo vyao.

“Mchakato wa amani na maridhiano unahitaji kuanzishwa upya,” Francis mwenye umri wa miaka 86, akasema kwenye hotuba yake katika Ikulu ya Rais jijini Juba, Sudan Kusini.

Alitaka juhudi kabambe ziendeshwe kukomesha kabisa katika taifa hilo changa zaidi duniani.

“Vizazi vijavyo, ama vitatukuza majina yenu au kuyafuta katika kumbukumbu zao, kwa misingi ya yale mnafanya sasa,” akaambia hadhira iliyowaleta pamoja Rais Salva Kiir, Naibu wake wa kwanza Riek Machar, wanadiplomasia, viongozi wa kidini na wafalme wa kitamaduni miongoni mwa watu wengine.

Tangu Sudan Kusini ilipotangazwa kuwa huru kutoka Sudan mnamo 2011, amani haijashuhudiwa katika nchi hiyo inayozongwa na umaskini.

Mwa miaka mitano, wanajeshi waaminifu kwa Kiir na wale ambao ni watiifu kwa Machar wamekuwa wakipigana. Mapigano hayo yamesababisha vifo vya watu 380,000 na wengine milioni nne wakafurushwa makwao.

“Mkomeshe umwagaji damu, mkomeshe vita na hali ya kulaumiana kuhusu ni nani mhusika. Msiwaache watu wenu na kiu ya amani. Wanataka amani haraka,” Francis akasema.

Ziara hiyo ya amani ni ya kwanza kwa Papa kufanya nchini Sudan Kusini tangu nchi hiyo – ambako raia wengi ni Wakristo – kupata uhuru kutoka Sudan yenye idadi kubwa ya Waislamu.

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki alitua nchini baada ya kufanya ziara ya siku nne katika nchini ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Vita vimechacha mashariki mwa nchini hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini.

Watu wengi, ambao walipiga foleni katika barabara za Jubaa kwa saa kadhaa kubla ya Papa kuwasili, walishangilia msafara wake uliopitia barabara zilizowekwa lami juzi.

Watu wengine walipiga magoti alipopita akiwapungia mkono.

Wengine walivalia mavazi ya kitamaduni au mavazi ya kidini, huku wengine wakipiga firimbi, kupuliza pembe na kuimba nyimbo za kikristo.

Kando na viongozi wa kisiasa, Papa Francis pia anatarajiwa kukutana na waathiriwa wa mapigano, viongozi wa makanisa na kuongoza ibada kubwa leo. Watu wengi wanatarajiwa kuhudhuria ibada hiyo.

Ziara hiyo ya Papa, ya tano barani Afrika, ilikuwa imepangiwa kufanyika 2022 lakini ikaahirishwa kwa baada ya Kiongozi huyo kukumbwa na tatizo la goti.

Tatizo hilo limefanya kutembea kwa kutumia viti vya magurudumu.

Mnamo 2019, Francis alitoa ahadi ya kuzuru Sudan Kusini alipokutana na Rais Kiir na Dkt Machar waliomtembea jijini Vatican. Aliwataka kuheshimu mkataba wa amani kwa manufaa ya raia wao.


    RAILA KUVUNA KWA VITA VYA RUTO NA UHURU

    KIONGOZI WA UPINZANI RAILA ODINGA

    VITA vipya vilivyochipuza kati ya Rais William Ruto na mtangulizi wake Uhuru Kenyatta huenda vikamfaidi kiongozi wa upinzani Raila Odinga katika vita vyake dhidi ya utawala wa Kenya Kwanza. Wadadisi wa masuala ya kisiasa sasa wanasema nipe nikupe hiyo kati ya Rais Ruto na Bw Kenyatta itampa Bw Odinga nguvu zaidi ya kuiponda serikali, kuiyumbisha na hata kuikosesha nafasi ya kutekeleza ahadi nyingi ilizotoa kwa Wakenya kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022. “Ikiwa joto hili la uhasama ambalo limechipuza tena kati ya Rais Ruto na Rais mstaafu halitapoeshwa kwa njia ya upatanisho, Raila ambaye ameanzisha msururu wa mikutano ya hadhara kote nchini ya kuipaka tope serikali hii changa atampa motisha mpya,” mchanganuzi wa msuala ya kisiasa Javas Bigambo amenukuliwa akisema. Anaongeza: “Raila atatumia nafasi hii kueneza ujumbe kwa wananchi kwamba serikali hii haina ajenda zozote za maendeleo zenye manufaa kwao ila inaongozwa na nia ya kulipiza kisasi dhidi ya wale aliowasawiri kama mahasidi wake, haswa, Rais Kenyattaa ambaye alimpokeza mamlaka kwa amani.” Akiongea mjini Mombasa Jumatatu alipofungua mkutano wa wabunge Rais Ruto alionekana kumshambulia Bw Kenyatta akidai ndiye amekuwa akifadhili mikutano ya Raila ya kupinga serikali ilia apate nafasi ya kukwepa kulipa ushuru. “Hata kama wanadhamini maandamano, ningetaka kuhakikishia kuwa sharti walipe ushuru. Sharti tuwe na nchi ambapo kila mtu analipa ushuru,” akasema, akiongeza: “Sirejelei ushuru mpya bali zile ambazo ni halali na zimeidhinishwa na Bunge. Rais alifananisha mienendo ya watu mashuhuri nchini, ambao hakuwataja, wa kukwepa ushuru na hali inayosawiriwa katika riwaya ya “Shamba la Wanyama” ambapo wanyama baadhi ya wanyama ni bora kuliko wengine. “Hatuko katika Shamba la Wanyama ambapo watu wengine ni bora kuliko wenzao. Sharti sote tulipe ushuru. Haijalishi idara ya mikutano ambayo utadhamini kuyumbisha ajenda yetu. Sharti ulipe ushuru,” akaongeza Dkt Ruto aliyeonekana mwenye ghadhabu. Rais alionekana kurejelea Bw Kenyatta, japo hakumtaja jina moja kwa moja. Lakini Rais huru mstaafu amejibu madai hayo akayataja kama “kilele za watu ambao wameshindwa kufanya kazi waliyopewa.” Rais Ruto alitoa kauli yake baada ya mwanablogu na mwanaharakati wa Kenya Kwanza Denis Itumbe kudai kuwa mikutano ya hadhara ya Bw Odinga inadhamini na “mtu fulani ambaye ambaye hataki watu walipe ushuru baada ya yeye na familia yake kukinga na sheria fulani kongwe kulipa ushuru kwa mali wanayomiliki.” Bw Itumbe aliweka mitandaoni sehemu ya Sheria ya zamani kuhusu Ardhi, “Estate Duty Act, Cap 483” iliyokinga familia za Rais wa kwanza Jomo Kenyatta na Rais wa Pili Daniel Arap Moi dhidi ya kulipa ushuru kwa ardhi kubwa zinazomiliki. Lakini baada ya Rais Ruto kutoa cheche kuhusu suala hilo la ushuru, maseneta watatu waliochaguliwa kwa tiketi ya chama cha United Democratic Alliance (UDA), John Methu (Nyandarua), James Murango (Kirinyaga na mwenzao wa Nyeri Wahome Wamatinga walimshambulia, moja kwa moja, Bw Kenyatta wakidai anatumia pesa alizokwepa kulipa kama ushuru kuhujumu serikali ya Kenya Kwanza. “Sisi kama viongozi tunaowawakilisha raia, hatuwezi kunyama huku mtu kama Rais mstaafu Uhuru Kenyatta akwepa ushuru na kutumia pesa hizo kufadhili maandamano na mikutano inayolenga kuvuruga amani nchini. Hivi karibuni tutadhamini mswada wa kubatilisha sheria hii inayokinga familia za Kenyatta na Moi dhidi ya kulipa ushuru,” akasema Bw Methu. Bila kutoa ithibati yoyote, maseneta hao waliochaguliwa kwa tiketi ya chama cha United Democratic Alliance (UDA) kinachoogozwa na Rais Ruto mwenyewe walidai kuwa wafadhili wa Azimio walifanya mikutano katika maeneo ya Maasai Mara, Mlima Kenya na Mombasa “kupanga njama zao za kuyumbisha serikali ya Kenya Kwanza.” Kwa upande mwingine, Seneta wa Nandi Samson Cherargei ameanzisha kampeni ya kumshinikiza Rais Ruto kumvua Bw Kenyatta wadhifa wa kuwa mpatanishi mkuu katika mchakato wa kuleta amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). “Rais Ruto anafaa kumpiga kalamu Bw Kenyatta kama balozi wa amani wa Kenya nchini DRC. Hawawezi kuendelea kutekeleza wajibu wa kuleta amani katika nchi hiyo ihali anafadhili fujo humo nchini,” Bw Cherargei akasema kupitia Twitter. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kenyatta Profesa Eric Masinde Aseka anasema kuwa kama Rais mstaafu, Bw Kenyatta anafaa kupewa heshima na mrithi wake. “Hizi vita ambavyo Uhuru anapigwa wakati huu bila shaka huenda ukaendeleza moto wa kisiasa ambao umeanzishwa na Bw Odinga kupitia mikutano yake ya kuipaka tope serikali ya Kenya Kwanza. Bilas haka Rais Ruto hataongoza kwa amani ikiwa ataonekana kama kiongozi anayeongozwa na nia na lengo la kulipiza kisiasa,” akaongeza mchanganuzi huyo wa masuala ya kisiasa.

    Tuesday 1 November 2022

    KOKO GAS COOKER TAKES BUNGOMA BY STORM!

     

    KOKO COOKER AT KSHS.3500     
    BY OUR TEAM
    A newly invented cooking  optional  apart from gas cylinder which has been in the market now for mor than two decades is facing a major blow after introduction of a new cooking machine which is so economical and people are running for it.

    ROUZY NELLY THE CHIEF AGENT BUNGOMA
    CONTACT:0791570802
    According to our research carried a week a go after meeting the chief agent Rouzy Nelly and some staff ,they explained to us how simple it is to be used by anybody anywhere.

    A product made from india has been now in the other part of the country  for now 3months.recently some of the  clients in bungoma have been  seriously looking for a way to dispose
    their cylinders for koko cooker.

    On interview with bungoma chief agent told us  some cartel are now taking the advantage of the market to kill the product by delivering half package  at expensive price leeding confusion of the  normal price of  kshs.3500

    Wednesday 8 June 2022

    ROGUE PASTOR JOHN LUTOMIA CORNING GAME EXPOSED

    John Lutomia
    A rogue missionary by the name John Lutomia  domaining  as John Lee is soliciting funds from hundreds of Kenyans in the name of helping them. According to our reliable source the man from luhya land who is now duping  the white men in the name of  helping valranable Africans  on different  capacity is believed  to be extracting money  as registration fee so as to be attended by the wazungus doctor which has remain as a dream to most victim .

    On the recent act the “man of God” had a bitter exchange of words in a whatsapp group  claiming to have helped achurch with kshs.80,000 that he even failed to  provide evidence. Also as we were making this report the rogue missionary has failed to pay back kshs.1300 to a cancer victim whom he duped  by the name simon oniang’o from vihiga county.

    In a whatsapp group the calprit who tried to outshine other members by posting  bundles of money  was put of as he pretend to  help by show of images of money.It is believed the man has been moving around trying  to dupe but it seems the milk is sour..
     

    Kenyans have been in the recent past fallen into such traps  after fake pastors who emails and get funds from abroad in the name of helping but turns up to be business practitioners  in the house of the lord. The matter is now being pursued by the authorities  to bring the culprit  to book.

    Tuesday 7 June 2022

    ROGUE PASTOR EXPOSED

                       

    JOHN LUTMIA 

    A rogue pastor who purport to be a missionary has been soliciting funds from innocent kenyans pretending to be helping them on different capacity. Sources told us the man by the name John Lutomia aka John Lee has is several occasion trying to use all means to extract  money from kenyans and emailing the Warungu's to be part of the mission. We have in possession credible information  about the rogue pastor that we shall publish by tomorrow