HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Wednesday 17 July 2024

SIMANZI KENYA JAJI OGEMBO AAGA DUNIA

Marehemu Jaji Daniel Ogembo, alipatikana Jumatano, Julai 17, 2024 akiwa ameaga dunia katika makazi yake rasmi mjini Siaya. Alitarajiwa kuongoza kikao asubuhi katika majengo ya Mahakama Kuu ya Siaya lakini akakosa kujitokeza hali iliyoibua shaka. Jaji Ogembo amehudumu kwa miaka miwili katika Mahakama Kuu ya Siaya alipokuwa jaji mkazi. Kamanda wa Polisi, Kaunti ya Siaya, Cleti Kimaiyo, alithibitisha kifo chake na kusema polisi na Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI) imeanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo. “Tutawafahamisha kuhusu matokeo, bado tunachunguza kiini cha kifo chake,” alisema mkuu wa polisi kaunti hiyo. Kulingana na afisa mmoja wa mahakama aliyechelea kutajwa kwa sababu ya uzito wa suala hilo, Jaji Ogembo alipatikana akiwa mfu asubuhi baada ya kukosa kujibu dereva wake alipokwenda kumchukua nyumbani kwake. “Dereva alimpeleka nyumbani Jumanne jioni lakini aliporejea asubuhi, jaji hakujibu hali iliyofanya dereva kuripoti kwa maafisa katika korti ya Siaya,” alisema afisa huyo wa ngazi ya juu. Kifo cha Jaji Ogembo kililemaza vikao vya korti huku wafanyakazi wakikumbwa na mshtuko kufuatia habari hizo. Kifo cha Jaji Ogembo kimetokea hata kabla ya wiki kuisha baada ya Jaji David Majanja kufariki dunia. Mwezi uliopita, Hakimu Mkuu wa Korti ya Makadara, Monicah Kivuti, aliuawa kwa kupigwa risasi na afisa mkuu wa polisi kutoka kituo cha Londiani.

No comments:

Post a Comment