HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Monday 5 August 2024

GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu wa Bangladesh, Sheikh Hasina Wazed amejiuzulu na kuondoka nchini humo, baada ya wiki kadhaa za maandamano yaliyoongozwa na wanafunzi na kupelekea machafuko makubwa nchini kote. Ripoti zinasema, bibi huyo mwenye umri wa miaka 76 alikimbia kwa helikopta Jumatatu hadi India, wakati maelfu ya waandamanaji wakivamia makazi yake katika mji mkuu wa Dhaka. Hilo limemaliza utawala wa Waziri Mkuu aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi nchini Bangladesh, kwa zaidi ya miaka 20 jumla. Anasifiwa kwa kusimamia maendeleo ya kiuchumi ya nchi hiyo ya Kusini mwa Asia, hata hivyo katika miaka ya hivi karibuni Bi Hasina ameshutumiwa kwa kugeuka kuwa kiongozi wa kiimla. Aliingiaje madarakani? Alizaliwa katika familia ya Kiislamu huko Bengal Mashariki mwaka 1947, Bi Hasina anatokea familia ya wanasiasa. Baba yake Sheikh Mujibur Rahman, 'Baba wa Taifa' la Bangladesh, alikuwa kiongozi mzalendo aliyeongoza uhuru wa nchi hiyo kutoka Pakistan mwaka 1971 na kuwa rais wa kwanza. Wakati huo, Bi Hasina alikuwa tayari anajuulikana kwa kuwa kiongozi wa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dhaka. Rahman aliuawa pamoja na watu wengi wa familia yake katika mapinduzi ya kijeshi mwaka 1975. Bi Hasina na dadake mdogo ndio pekee walionusurika kwani walikuwa safarini nje ya nchi wakati huo. Baada ya kuishi uhamishoni nchini India, Bi Hasina alirejea Bangladesh mwaka 1981 na kuwa kiongozi wa chama cha kisiasa cha babake, Awami League. Aliungana na vyama vingine vya kisiasa kufanya maandamano mitaani ya kuunga mkono demokrasia, wakati wa utawala wa kijeshi wa Jenerali Hussain Muhammed Ershad. Vuguvugu hilo lilimfanya Bi Hasina akawa mwanasiasa wa kitaifa haraka sana. Aliingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 1996. Alipata sifa kwa kutia saini mkataba wa kugawana maji na India na mapatano ya amani na waasi kusini-mashariki mwa nchi hiyo. Lakini wakati huo huo, serikali yake ilikosolewa kwa mikataba mingi ya kibiashara inayodaiwa kuwa ni mbovu na kwa kuwa mtiifu sana kwa India. Baadaye alishindwa na mshirika wake wa zamani aliyegeuka kuwa mpinzani, Bi Begum Khaleda Zia wa chama cha Bangladesh Nationalist Party (BNP), mwaka 2001. Wanawake wote wawili wametawala siasa za Bangladesh kwa zaidi ya miongo mitatu na wanajulikana kama "Begums wanaovutana." Begum ina maana ya mwanamke wa Kiislamu wa daraja la juu. Waangalizi wanasema ushindani wao mkali umesababisha mlipuko wa mabomu katika mabasi, kutoweka na mauaji ya kiholela ya mara kwa mara. Bi Hasina hatimaye alirejea mamlakani mwaka 2009 katika uchaguzi uliofanyika chini ya serikali ya mpito. Akiwa mwathirika wa kisiasa, amekamatwa mara kadhaa akiwa upinzani na vile vile majaribio kadhaa ya kumuua, likiwemo moja la mwaka 2004 ambalo liliharibu usikivu wake. Pia amenusurika juhudi za kumlazimisha Kwenda uhamishoni kwa kesi nyingi mahakamani zinazomshutumu kwa ufisadi. Mafanikio yake ni yapi? Bangladesh, taifa lenye Waislamu wengi, lilikuwa mojawapo ya mataifa maskini zaidi duniani, limepata mafanikio makubwa ya kiuchumi chini ya uongozi wake tangu 2009. Sasa ni moja wapo ya taifa lenye uchumi unaokua kwa kasi katika eneo hilo, hata kupita jirani yake mkubwa India. Pato la taifa kwa mtu mmoja limeongezeka mara tatu katika muongo uliopita na Benki ya Dunia inakadiria kuwa zaidi ya watu milioni 25 wameondokana na umaskini katika miaka 20 iliyopita. Sehemu kubwa ya ukuaji huu imechochewa na sekta ya nguo, ambayo inachangia idadi kubwa ya mauzo ya nje ya nchi na sekta hiyo imekuwa katika miongo ya hivi karibuni, ikisambaza nguo katika masoko ya Ulaya, Amerika Kaskazini na Asia. Serikali ya Bi Hasina imefanya miradi mikubwa ya miundombinu kwa kutumia fedha za nchi hiyo, mikopo na usaidizi wa maendeleo, ikiwa ni pamoja na daraja kubwa la Padma lililogharimu dola za kimarekani bilioni 2.9 huko Ganges.

No comments:

Post a Comment