HABARI KUU:

Mamia ya wanafunzi, wazazi, walimu na wahitimu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Peters Mwiruti katika Kaunti Ndogo ya Bumula, Kaunti ya Bungoma, walijaa katika uwanja wa shule kusherehekea baada ya kutangazwa kwa matokeo ya mtihani wa KCSE wa mwaka 2025, ambapo shule hiyo ilivunja rekodi yake ya awali ya kitaaluma..//..NAIROBI, KENYA, Alhamisi, Januari 1, 2026 – Kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM), Oburu Oginga, ametangaza wazi kuwa atakuwa mgombea wa urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2027 endapo ODM itaamua kugombea pekee bila kuingia muungano na vyama vingine..//..NAIROBI, KENYA, Jumanne, Januari 6, 2026 – Zaidi ya viongozi 42 wa matawi ya vyama vya wafanyakazi vilivyoambatanishwa na COTU-K wametangaza kumunga mkono mwenyekiti Francis Atwoli wakati anapojitayarisha kuwania muhula mwingine, utakaomfikisha zaidi ya miongo miwili madarakani.

Monday, 5 August 2024

AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA

WANAFUNZI 26, walimu watatu na mpishi mmoja wa shule ya Rockside Academy, Nairobi wanapokea matibabu katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Nakuru na Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Molo baada ya gari lao kuhusika katika ajali eneo la Sachangwan, Nakuru, Jumatatu, Agosti 5, 2024. Kwa mujibu wa Kamanda ya Polisi wa Kaunti Ndogo ya Molo Timon Odingo, basi hilo la shule lilikuwa likiwasafirisha wanafunzi kutoka Eldoret ambako walikuwa wameshiriki tamasha za muziki zinazoendelea. Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa saba za mchana baada ya lori kutoka nyuma kupoteza mwelekeo na kugonga basi hilo kutoka nyuma. Baadaye lori hilo liligonga magari mengine mawili ya kibinafsi hadi yakaanguka kwenye mtaro kando ya barabara. Watu 30 walipata majeraha katika ajali hiyo, japo waliokuwa kwenye magari ya kibinafsi hawakuathiriwa. Maafisa wa polisi walipowasili katika eneo la ajali wenyeji na wasamaria wema walikuwa tayari wamewaondoa waathiriwa. “Waliojeruhiwa wamekimbizwa hospitalini na sasa wanapokea matibabu. Kwa bahati nzuri hakuna aliyekufa. Maafisa wa polisi wametumwa hospitali kuendeleza uchunguzi,” Bw Odingo akasema.

No comments:

Post a Comment