HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Monday 16 September 2024

WANAFUNZI WA ZAMANI WA MANORHOUSE WAOMBOLEZA KIFO CHA BABA WA MWENZAO

 


Wingu la majonzi ligubika jamii ya zamani ya shule ya upili ya manorhouse baada ya mmoja wao kumpoteza babake.Wycliff Chonge ambaye alikuwa kiongozi wa muungano wa dini katika shule hiyo alimpoteza babake Mzee Chonge akimtaja kama mtu aliyekuwa mzazi na rafiki aliyesimama naye katika kuishi kwake.

Wanafunzi wa zamani wa shule hiyo wameendelea kutuma risala za rambirambi kutoka kila pembe ya nchi.Umoja wao umetokana na vifo vilivyofuatana ikiwemo wa mkewe  phillip simiyu alifariki kutokana na ajali ya barabarani na kuzikwa kule cheranganyi na kifo cha babake peter kunania miezi michache iliyopita.

Kufikia sasa shughuli ya mipango ya mazishi inaendelea kwa kasi  huku kamati mbalimbali zikiundwa.Hizi ni baadhi rambirambi zilizotumwa....

PTER KUNANIA-May God give you strength bro,ni ngumu but take heart,pole sana,it is well my brother

PHILIP SIMIYU-Brother Wicky, Pole sana for the loss of your dearest friend, father,  and mentor may the good lord give the Chonges strength and peace at this trying moment. Rest in peace mzee.

N.K-So sorry for the loss of dad brother Wicky........may God strengthen you at this trying moments, be strong in the Lord.

JOSODOKE-Oh no! 😔 Pole Chairman.May God give you strength to bear this big loss.I have been there also and I know it's not easy😌.May God come through for you and your family

KIZITO-Pole chairman for the loss of your, May Almighty God give enough comfort at this low moments of your life

LINNET CHIRCHIR-My condolences to our brother Wycliffe chonge.May the good lord comfort your family at large in a special way

GILHAGE-Condolences to Chonge and family may the Almighty God strengthen you during this difficult period.

CHOZEN MWANGI-My condolences to chairman chonge and family

EUNICE NJERI-My condolences dear brother for this trying moment it's not easy but my almighty God comfort u n ur family


RAIS AKAIDI NA KUENDELEZA MICHANGO KANISANI HUKU AKITOA KSHS.1O MILION

 


RAIS William Ruto amefeli kudhihirisha kwa vitendo hatua yake ya kuzima maafisa wa serikali kushiriki michango ya harambee kama mojawapo ya njia za kupambana na ufisadi.

Alitoa agizo hilo Julai 2024 ili kuzima maandamano ya vijana wa Gen Z waliolalamika kuwa hulka ya viongozi na maafisa wakuu serikalini ya kutoa pesa nyingi katika michango hiyo inaendeleza uovu huo.

Wakati huo, Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi, ambaye ni mwandani wa Rais Ruto, alishutumiwa kwa kutoa Sh20 milioni, wakati mmoja, katika harambee, watu wakihoji asili ya pesa hizo.

Lakini Jumapili, Septemba 15, 2024, saa chache baada ya kuwasili nchini kutoka ziara rasmi nchini Ujerumani, Dkt Ruto pamoja na wandani wake walihudhuria Ibada katika Kanisa la Stewards Revival Pentecostal, Nairobi.

Wakati wa ibada hiyo, Rais alijitolea kusaidia katika ujenzi wa jengo jipya katika kanisa hilo baada ya jengo la zamani kubomolewa kutoa nafasi kwa upanuzi wa barabara ya Outering.

Aliahidi kutoa mchango wa Sh10 milioni kufadhili mradi huo licha ya kufahamu fika kuwa wananchi wanachukia mienendo ya viongozi kutoa michango ya aina hiyo, hali iliyolazimisha serikali kuidhibiti.

“Najulikana zaidi kama mshirika mkubwa katika miradi ya ujenzi wa makanisa. Unishirikishe hapo…….. Nimekubaliana na Askofu na nitatoa Sh10 milioni kufadhili ujenzi huu,” Rais Ruto akasema waumini wa kanisa hilo wakishangilia kwa furaha.

Hata hivyo, Rais alijaribu kufafanua kwamba kile alichofanya haikuwa harambee, bali ni “mchango tu”.

“Sharti tujenge kanisa hili kwa neema ya Mungu, tatakuja hapa kuizindua,’ akasema kiongozi wa nchi.

Alipokuwa akitangaza hatua ambazo serikali yake imeweka kuzuia maafisa wakuu na watumishi wa umma kushiriki michango ya harambee, Rais Ruto aliagiza Mwanasheria Mkuu kubuni sheria ya kufanikisha hatua hiyo.

STARLINK YAIMARISHA USHINDANI


 MKURUGENZI Mkuu mteule wa Mamlaka ya Ushindani Nchini (CAK) David Kemei amewahakikishia Wakenya kwamba atazima mjadala kuhusu kampuni ya kutoa huduma za intaneti ya Sterlink baada ya Bunge kuidhinisha uteuzi wake.

Bw Kemei ambaye anatarajiwa kupigwa msasa na Kamati ya Pamoja ya Bunge la Kitaifa na Seneti kuhusu Fedha Jumanne, Septemba 17, 2024 alisema atashirikisha sekta zote katika kuleta maridhiano kati ya Starlink na kampuni zingine zinazotoa huduma hiyo nchini.

Kwenye mahojiano na Taifa Dijitali, Bw Kemei alisema anaelewa malalamishi yaliyowasilishwa dhidi ya kampuni hiyo ya Amerika na kampuni za humu nchini haswa Safaricom

“Hauwezi kutoa idhini kiholela. Sharti uangalie masuala yote, ushirikishe kampuni zote husika kabla ya kutoa mwelekeo utakaowafaa wadau hao wote,” Bw Kemei akasema.

Hata hivyo, mkurugenzi huyo mteule alizitaka kampuni za humu nchini na wadau wengine katika sekta ya mawasiliano kukumbatia teknolojia bora ili kuimarisha huduma kwa Wakenya.

“Uzuri wa ujio wa Starlink ni kwamba utazilazimu kampuni za hudumu nchini kuwa wabunifu na kukumbatia mbinu za kisasa katika utoaji huduma. Tunataka kampuni za hapa nchini zitikiswe ili zitupe huduma bora, ndipo kusema ni kampuni inayotangaza faida ya mabilioni ya fedha ilhali maeneo mengine ya nchi hayajaunganishwa na intaneti,” Bw Kemei akasema

Alisema kuwa atahakikisha kuwa wadau wote wameshirikishwa katika kupatikana kwa mwafaka kuhusu suala hilo kuhakikisha kuwa kila mtu anapata nafasi ya kuhudumu huku kampuni za humu nchini zikilindwa dhidi ya ushindani usiofaa.

Kulingana na Bw Kemei, baadhi ya kampuni za humu nchini zimewekeza mabilioni ya fedha katika miundomsingi, rasilimali ambazo haziwezi kuruhusiwa zifutiliwe na ujio wa kampuni mpya ya kutoa huduma za intaneti.

Alisema masuala kama vile usalama wa nchini na ulinzi wa data yanapaswa kuzingatiwa kabla ya kuidhinisha Starlink kutoa huduma za intaneti kwa Wakenya.

Sunday 15 September 2024

WAKENYA WAONGEZEKA JELA ZA MAREKANI

 


UFICHUZI wa hivi majuzi wa kukamatwa na kufungwa kwa aliyekuwa mgombea urais Mohamed Abduba Dida unaongeza orodha ya raia wa Kenya wanaotumikia kifungo jela nchini Amerika.

Mwalimu huyo wa zamani ambaye aliwania urais mwaka wa 2013 na 2017 kwa sasa anazuiliwa katika gereza la Big Muddy huko Illinois baada ya kupatikana na hatia ya kumnyemelea na kumtisha mkewe waliyetengana.

Wakenya wengine mashuhuri waliozuiliwa nchini Amerika ni wana wawili wa Akasha waliopatikana na hatia ya ulanguzi wa dawa za kulevya na pia kuzuia haki kwa kutoa hongo kwa maafisa wa Kenya katika jitihada za kuepuka kupelekwa Amerika kushtakiwa.

Baktash Akasha alihukumiwa kifungo cha miaka 25 jela mwaka wa 2019 huku Ibrahim Akasha akihukumiwa miaka 23 mnamo 2020.

Ndugu hao wa Akasha walikamatwa Mombasa mnamo Novemba 2014 katika oparesheni iliyoongozwa na Amerika.

Huenda kifungo kirefu zaidi ni cha Brian Musomba Maweu aliyehukumiwa kufungwa jela maisha mwaka 2015 kwa kuhusika na ponografia ya watoto.

Mwaka wa 2014, alichapisha jumbe 121 kwenye tovuti ya Dreamboard–mtandao wa kibinafsi wa wanachama pekee ambao ulikuza unyanyasaji wa kingono na unyanyasaji wa watoto wadogo.

Kevin Kang’ethe ambaye aligonga vichwa vya habari baada ya kutoroka kituo cha polisi pia sasa anazuiliwa gerezani nchini Amerika baada ya kurejeshwa humo wiki mbili zilizopita.

Anakabiliwa na kesi ya mauaji ya kinyama ya mpenzi wake Margaret Mbitu mwaka jana, 2024. Alitoroka Amerika hadi Kenya baada ya kufanya uhalifu huo lakini maafisa walifuatilia na kumkamata.

Akiwa kizuizini katika kituo cha polisi cha Muthaiga, alitoroka katika hali isiyoeleweka na alikamatwa tena na kurudishwa Amerika kwa ndege ya kibinafsi ya FBI kujibu mashtaka ya mauaji.

Mnamo Septemba 3, 2024 alikana mashtaka na amepangwa kurejea kortini Novemba 5 kesi kusikilizwa. Anazuiliwa bila dhamana.

Ulaghai ukiwemo ulaghai wa mapenzi na ulaghai wa uwekezaji ni baadhi ya uhalifu ambao umepelekea baadhi ya Wakenya kufungwa gerezani Amerika siku za hivi majuzi.

Mnamo Februari Paul Maucha, 59, alipatikana na hatia ya njama ya kuwalaghai watu kwa kuwahadaa walipe pesa kwa kampuni kwa kisingizio kwamba wangepokea faida nzuri za kifedha baadaye.

Mwaka jana, 2023, Florence Mwende Musau alifungwa jela kwa kushiriki katika njama iliyohusisha ulaghai wa mapenzi iliyobuniwa kuwahadaa waathiriwa kutuma pesa kwa akaunti za benki zilizodhibitiwa naye na watu wengine.

Alipatikana na hatia ya kutumia pasipoti ghushi zenye majina tofauti kufungua akaunti za benki ambapo angepokea pesa kutoka kashfa za mapenzi.


Mnamo Mei 2023, mahakama ilimhukumu Abdi Hussein Ahmed kifungo cha miaka minne kwa kula njama ya kusafirisha kiasi kikubwa cha pembe za kifaru na pembe za ndovu za thamani ya mamilioni ya pesa.

Pia, alipatikana na hatia ya kulangua heroin.

Mnamo Januari, Erick Gachuhi Wanjiku, 42, alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuwashambulia maafisa wa serikali.

MOTO WATEKETEZA SHULE MACHAKOS JUMAPILI

MKASA wa moto umeripotiwa katika Shule ya Upili ya Katoloni iliyoko Kaunti ya Machakos. Kulingana na Shirika la Msalaba Mwekundu Nchini (KRC), moto huo ulitokea dakika chache baada ya saa tatu za usiku wa Jumamosi, Septemba 14, 2024. “Kisa cha moto kimeripotiwa katika Shule ya Upili ya Katoloni iliyoko Kaunti ya Machakos. Juhudi za kuuzima zinaendelea,” KRC ikasema kwenye ujumbe kupitia akaunti yake ya X. Hata hivyo, baadaye wafanyakazi wa shirika hilo la kushughulikia majanga wakishirikiana na wale wa Idara ya Zimamoto katika serikali ya Kaunti ya Machakos walifaulu kudhibiti na kuzima moto huo. “Shirika la Msalaba Mwekundu pia linatoa huduma ya kwanza katika eneo la tukio,” KRC iliandika kwenye X, baada ya muda wa saa tatu. Duru zinasema kuwa wanafunzi wawili walikimbizwa katika Hospitali ya Machakos Level 5, baada ya kuathiriwa na moshi uliotokana na moto huo. Visa kadhaa vya moto kuteketeza mali vimeripotiwa katika shule kadha nchini mwezi huu wa Septemba. Mkasa mbaya zaidi ulikuwa ni ule uliotokea usiku wa kuamkia Ijumaa, Septemba 6, 2024 Hillside Endarasha Academy, Nyeri ambapo jumla ya wanafunzi 17 walikufa papo hapo. Wengine wanne walikufa hospitalini kutokana na majeraha ya moto na hivyo kufikisha idadi jumla ya waliokufa kuwa 21.

Saturday 14 September 2024

GEN Z WAAPA KUSIMAMA NA GACHAGUA

 


VIONGOZI wa vijana kutoka Mlima Kenya wamewashutumu Wabunge  ambao wamejitenga na Naibu Rais Rigathi Gachagua na kumwidhinisha Waziri wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki kuwa Msemaji wa eneo hilo.

Wakiongozwa na Mtaalamu wa Usawa wa Jinsia, Dkt Fridah Karani, viongozi hao walishutumu wabunge hao kwa kujihusisha na siasa za migawanyiko badala ya kuangazia maendeleo ya eneo hilo.

Walijitenga na wabunge hao, wakisema hawakushauriwa.’Hakukuwa na ushiriki wa umma na kwa hivyo tunakataa uamuzi wa wabunge,’ alisema Dkt Karani.

Vijana waliapa kupinga hatua yoyote ya kugawanya eneo hilo.’Sisi kama vijana, hatuwezi kusimama na kutazama jinsi siasa za migawanyiko na ajenda za ubinafsi zinatishia umoja wetu, utulivu na maendeleo,’ alisema.

Vijana walisisitiza kuwa ajenda ya mgawanyiko inayoenezwa na wabunge inaonyesha kutojali kabisa usawa wa kijinsia na maendeleo ya eneo lao.

‘Vijana na wanawake wanatengwa katika mijadala muhimu ya kisiasa licha ya kikatiba kuamuru kujumuishwa kwao,’ alisema Dkt Karani.Wabunge 14 kutoka kaunti za Embu, Meru na Tharaka Nithi walitangaza kwamba Prof Kindiki atakuwa msemaji wao wa kuuunganisha eneo hilo na serikali ya Rais William Ruto.

Mnamo Alhamisi, wabunge 48 wa eneo la Mlima Kenya Magharibi pia walijitenga na Bw Gachagua na kumuunga Profesa Kindiki kuwa msemaji wao.

Wabunge walisema wameungana kushawishi maendeleo ya Mlima Kenya.

“Kama viongozi waliochaguliwa kutoka Mlima Kenya, kwa niaba yetu na wakazi waliotuchagua, tumeamua kuwa atakayetuunganisha na serikali kuu ni Profesa Kindiki,” walisema katika taarifa.

Wabunge hao wanaotoka kaunti za Kiambu, Murang’a, Nyeri, Nyandarua, Kirinyaga, Nakuru, Laikipia na Nairobi, walisema<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-5352755744671694"

     crossorigin="anonymous"></script> Bw Gachagua ameshindwa kuonyesha uongozi bora na kukataa kuungana na Rais kuwaunganisha Wakenya.

“Juhudi zetu za kusaka maendeleo kwa watu wetu zimetatizwa na kukosekana kwa kiongozi ambaye anatuelewa na anayeweza kupeleka maslahi ya watu wetu kwa serikali kuu.

“Hata hivyo, Seneta wa Kirinyaga Kamau Murango na Mwakilishi wa Wanawake Njeri Maina wamejitenga na wabunge hao wakisema hawakuhusisha maoni ya wakazi wa eneo hilo. Walisisitiza kuwa wabunge hao wamepoteza mwelekeo wa kisiasa, wakionya kuwa huenda wakapoteza viti vyao katika uchaguzi ujao. Wabunge hawa wamekosea na wakazi kutoka eneo hili hawajafurahishwa nao,’ alisema Bw Murango.

Bi Maina alitaja hatua ya wabunge hao kama aibu kwa eneo lao.

‘Naibu Rais ndiye mwanasiasa mkuu kutoka eneo letu lakini cha kusikitisha ni kwamba wabunge wanapigana naye,’ alisema.

Bi Njeri aliapa kuendelea kumuunga mkono Bw Gachagua ambaye alisema ana nia nzuri kwa eneo la Mlima Kenya.

‘Adui zangu wa kisiasa wananiita mfuasi shupavu wa Bw Gachagua. Ni kweli na nitaendelea kumuunga mkono kwa sababu ni kiongozi mzalendo wa Milimani,’ alisema Bi Njeri.


MTOTO ATOBOA KUWA BABAKE AMEFARIKI KISUMU HUKU BIW SAMINZI LIKITANDA

 

KIINI cha mwanaume mwenye umri wa miaka 39 kujiua akiwa nyumbani mwake Manyatta viungani mwa jiji la Kisumu kingali kitendawili kwa jamaa na majirani.

Kinachojulikana kufikia sasa ni kuwa Washington Obat aligombana na mkewe Caroline Achieng mara kadhaa Alhamisi kabla ya tukio hili la kutatanisha kusababisha wingu la simanzi kutanda eneo la Manyatta.

Mke wa marehemu anasimulia kuwa walikuwa na mzozo Alhamisi jioni.

Baada ya mzozo, mume wake alimwomba msamaha warudieni na kuendeleza familia.

Ilikuwaje baadaye Obat ‘alijitia kitanzi’?

Mzozo mkali

Mkazi huyu wa Wadi ya Kondele anafichua kuwa walikabiliana vikali na mumewe katika patashika iliyomsabibishia majeraha mwilini.

Kulingana na Achieng’, isingalikuwa shangazi za mume wake, pia yeye angekuwa marehemu kama mume wake.<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-5352755744671694"

     crossorigin="anonymous"></script>

“Kwa bahati nzuri niliokolewa na shangazi zake na ilibidi nilale kwa majirani kuepuka hatari zaidi,” alisimulia.

“Alikuja kwa familia yangu na kunishawishi kwamba turudi nyumbani na tukapatana. Baadaye aliondoka kuelekea kazini lakini alirudi akiwa mlevi na kuanza kunisumbua huku akiniuliza nina tatizo gani. Hapo ndipo alifunga mlango na kuanza kunipiga. Nilijaribu kutoroka na kuripoti katika kituo cha polisi cha Manyatta.”

Achieng anaeleza kwamba alimtuma mwanawe nyumbani kwao kuchukua sare za shule.

Kwa bahati mbaya, anasema, mtoto wake alikutana na mwili wa baba ukilala bila pumzi.

“Nilikuwa nimemtuma mwanangu aende kuchukua sare yake kutoka nyumbani Ijumaa asubuhi lakini alimkuta baba yake tayari amekufa,” alisema.

Chifu Msaidizi wa Kata ndogo yaa Manyatta A, Agnes Akinyi alithibitisha kisa hicho na kufichua kuwa ripoti hiyo ilitumwa kituoni na mzee wa kijiji cha eneo hilo Isaac Opiyo.

“Tulipokea ripoti kutoka kwa mzee wa kijiji chetu Opiyo, kwamba mwanamume anayejulikana kama Washington Obat amejiua kufuatia ugomvi wa kifamilia,” Akinyi alifichua.

Chifu huyo msaidizi alitoa wito kwa wanandoa kutafuta usaidizi kutoka kwa afisi za serikali na mashirika mengine ya eneo hilo wakati wowote ndoa zao zinaingia doa.

Aliwaonya wanandoa dhidi ya kujichukulia sharia mkononi.

“Ikiwa wanandoa wanatofautiana basi ni bora kutafuta suluhu ya amani badala ya kujitoa uhai kwa sababu hiyo si suluhu,” alitanguliza. “Ombi langu kwa wanandoa ni kuwa karibu na afisi za serikali ili kusaidia kutatua masuala yao,”

Kadhalika, Bi Akinyi aliwahimiza wakaazi kutambua dalili za mizozo inayoweza kuwaletea balaa baadaye.

Wanapotambua changamoto za awali, aliendelea, wanafaa kushirikiana na kuhusisha uongozi wa mtaa kuwasaidia.

Monday 9 September 2024

MKUU WA BARAZA LA MAWAZIRI MSALI MUDAVADI AELEKEA NAMIBIA KUMPIGIA DEBE RAILA- AUC


 MKUU wa Mawaziri na Waziri wa Masuala ya Kigeni Musalia Mudavadi anaelekea Namibia ambako anatarajiwa kumpigia debe Raila Odinga katika azma yake ya kutaka achaguliwe mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).

Bw Mudavadi, ambaye aliondoka Jumapili pia ameratibiwa kufanya mashauriano na viongozi wakuu wa Namibia akilenga kuimarisha mahusiano kati ya Kenya na nchi hiyo katika nyanja kadhaa za kimaendeleo.

Hata hivyo, afisi yake ilisema kwenye taarifa kwamba ajenda kuu ya ziara yake ni kumpigia debe Bw Odinga atakapokutana Makamu wa Rais wa Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah.

“Mudavadi atatumia nafasi hiyo kuvumisha azma ya Raila Odinga katika kinyang’anyiro cha uenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC) mnamo Februari 2025,” ikasema taarifa iliyotumwa kwa vyombo na Mkurugenzi wa Kitengo cha Habari katika afisi ya Mudavadi Jacob Ng’etich.

Ziara hii ni ya kwamba ya kusaka uungwaji mkono kwa Bw Odinga katika eneo la Afrika Kusini baada ya kuzinduliwa kwake jijini Nairobi.

Hafla hiyo iliyofanyika katika Ikulu ya Nairobi ilihudhuriwa na baadhi ya marais wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Kenya imewasilisha mwaniaji wa uenyekiti wa AUC kwa mara ya pili mfufulizo baada ya aliyekuwa Waziri wa Masuala ya Kigeni Amina Mohamed kushindwa na mwenyekiti anayeondoa Moussa Faki Mahamat mnamo 2017.

Bw Odinga anashindana na wagombeaji wengine watatu ambao ni Waziri wa Masuala ya Kigeni wa Djibouti Mohamoud Ali Youssouf, aliyekuwa waziri wa masuala ya kigeni wa Mauritius Anil Kumarsigh Gayan na Waziri wa zamani wa Masuala ya Kigeni wa Madagascar Richard Randriamandrato.

Hata hivyo, inabashiriwa kuwa Youssouf ambaye amehudumu kama Waziri wa Masuala ya Kigeni kwa miaka 10 ndiye mshindani mkuu wa Bw Odinga.

Ziara ya Mudavadi nchini Namibia inajiri baada ya Bw Odinga kuungana na ujumbe wa Rais William Ruto katika mkutano wa mashauriano kati ya marais wa Afrika na China kuhusu masuala ya maendeleo (FOCAC) wiki jana jijini Beijing, China.

Wakati wa mkutano huo, Rais Ruto alifanya mikutano tofauti na marais sita wa Afrika kumpigia debe Bw Odinga.

Kando na kumfanyia kampeni Bw Odinga, Bw Mudavadi anatarajiwa kutetea kuimarishwa kwa mahusiano kati ya Kenya na Namibia na kuanzisha kwa ubalozi wa Kenya jijini Nairobi.

Aidha, atatetea kuimarishwa kwa biashara kati ya Kenya na Namibia kwa manufaa ya nchi hizo mbili.

Kulingana na ripoti kutoka kwa Wizara za Masuala ya Kigeni na Biashara nchini Kenya imekuwa ikiagiza bidhaa za thamani ya Sh117.76 milioni kutoka Namibia na kuuza bidhaa za thamani ya Sh106.31 milioni nchini Namibia ndani ya kipindi cha mwongo mmoja.

Imetafsiriwa na Charles Wasonga 

KENYA:DCI YAANZISHA UCHUNGUZI KUHUSU MKASA WA MOTO ULIOTEKETEZA WANAFUZI 21 HADI KIFO


 MAAFISA wa upelelezi wanakusanya maelezo yanayotarajiwa kusaidia kutegua kitendawili kuhusu chanzo cha moto kilichosababisha vifo vya wanafunzi 21 katika Shule ya Hillside Endarasha Academy, Kieni, Nyeri.

Miili ilipelekwa katika Hifadhi ya Maiti ya Hospitali ya Naromoru Level Four kufanyiwa ukaguzi na vipimo vya chembechembe za DNA kuitambua.

Mwanapatholojia wa serikali Dkt Johansen Oduor, Jumapili alisema vipimo vya DNA vitaanza kufanywa, Jumatatu, Septemba 9, 2024.

Jumapili, wahudumu katika hifadhi hiyo ya maiti walikuwa wakiandaa miili hiyo kabla ya wanapatholojia kuwasili.

Hifadhi hiyo inaendelea kujengwa na haijakamilika.

Maswali

Maswali yameulizwa kuhusu chanzo cha moto huo japo madai yameibuliwa kuwa huenda ulisababishwa na kulipuka kwa balbu ya stima.

Hata hivyo kuna wazazi ambao wamepinga nadharia hiyo, wakidai Alhamisi wanafunzi walidaiwa kuibua malalamishi kuhusu masuala fulani shuleni humo.

Mzazi aliyeongea na Taifa Leo Dijitali, na akaomba tulibane jina lake, alisema alipata habari hizo kutoka kwa mwanawe ambaye ni mwanafunzi wa kutwa.

Alisema mvulana huyo  wa Gredi 7, alimweleza kuwa mwendo wa saa kumi za jioni baadhi ya wanafunzi walikaa “kwa muda mrefu” katika bweni lililoteketea “wakijadili masuala fulani” ambayo sio ya kawaida.

Usimamizi wa shule hiyo haujatoa taarifa zozote tangu kutokea kwa mkasa huo.

“Baadhi ya wanafunzi walikaa kwa muda mrefu katika bweni na mwanangu aliniambia kulikuwa na wasiwasi shuleni kuhusu mambo yasiyojulikana.

Watoto huwa hawaruhusiwi kwenda katika bweni nyakati za mchana. Wakitaka kwenda huko, sharti waandamane na msimamizi wa mabweni wachukue kile wanachotaka kisha warejee madarasani mara moja. Mbona kanuni hii haikuzingatiwa?”, akauliza.Mzazi huyo pia alisema kuwa mwendo wa saa  nne usiku, kuna mwanafunzi aliyempigia simu mzazi wake na kupasha habari kuhusu kutokea kwa moto.

“Swali ni je, simu hiyo ilikuwa ya nani na ni mzazi yupi huyu alipigiwa simu?” mzazi huo akauliza.

“Tunafahamu fika kwamba watoto hawaruhusiwi kutumia simu za mkono wakiwa shule na hufanya hivyo tu baada ya kupata kibali maalum na chini ya usimamizi wa mwalimu mhusika. Tunataka mzazi huyu aliyepigiwa simu ajitokeze na kutoa maelezi kwa maafisa wa upelelezi ili ibainike kilichotendeka.” Mzazi huyo akasema.

Maafisa hao wa upelelezi wa vifo, wakiongozwa na Martin Nyuguto, waliendelea kusaka ushahidi katika eneo la mkasa huku serikali ikisema watoto 48 bado hawajulikani waliko kufikia Jumapili, Septemba 8, 2024 jioni.

Lakini Ijumaa Septemba 6, 2024, Naibu Rais Rigathi Gachagua alisema watoto 70 hawakujulikana waliko.

Alibashiri kuwa walipewa hifadhi katika makazi  ya karibu na Shule ya Hillside Endarasha Academy, walikokimbilia moto ulipotokea.

Jumapili, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki jimbo la Nyeri, Anthony Muheria, alitoa wito kwa wazazi waliwachukua watoto baada ya mkasa kupiga ripoti kwa maafisa wa usalama ili kuzima dukuduku kuhusu idadi ya watu ambao hawajulikani waliko.

“Ikiwa mtoto wako yuko nyumbani wapashe maafisa wa upelelezi ili wajue kwamba wako salama. Watoto hao pia wanafaa kupewa ushauri nasaha kutokana na mshtuko uliowapata wakati wa mkasa huo wa moto,” Askofu Muheria akasema wakati wa ibada ya pamoja na kuombea waliofuka na kuzifariji jamaa zilizopoteza watoto wao.

MAANDAMANO YA WANAFUNZI KENYA

Mmoja wa wanafunzi wa somo la udaktari katika Chuo Kikuu cha Moi waliandamana mjini Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu, kupinga mfumo mpya wa ufadhili wa elimu ya chuo kikuu mnamo Septemba 9, 2024. PICHA | JARED NYATAYA

 WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Moi bewa kuu la  Kesses mjini Eldoret waliandamana Jumatatu wakitaka kufutiliwa mbali au kubadilishwa kwa mfumo mpya wa ufadhili wa masomo ya chuo kikuu.

Yalijiri licha ya viongozi wa kitaifa wa wanafunzi wa vyuo vikuu kupiga breki maandamano waliyopanga kufanya kote nchini kuanzia wiki hii, baada ya serikali kuahidi kwamba ungetathmini upya mfumo huo wa kufadhili elimu ya juu.

Hata hivyo, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Moi walishiriki maandamano kwa kuimba nyimbo za kupinga serikali na kubeba mabango yaliyopinga mtindo huo mpya wa ufadhili. Waliwataja viongozi wao wa kitaifa kama wasaliti.

 “Kama Chuo Kikuu cha Moi tunashikilia msimamo wetu kwamba tunakataa mtindo huu wa ufadhili. Siku 30 ambazo serikali imeomba ili kutathmini upya mfumo huo ni njama ya kutufumba macho hadi mwisho wa muhula wa sasa wa masomo,” alisema Enock Kwena mmoja  wa viongozi wa wanafunzi katika chuo hicho.

Wanafunzi hao walishutumu serikali kwa kutojali masaibu ya wanachuo.

Walisema hawana imani kamwe na utawala wa sasa na hususan ahadi iliyotolewa na Waziri wa Elimu Julius Ogamba; ya kuundwa kwa kamati mbili zitakazotathmini mfumo huo mpya wa ufadhili, akitoa wito kwa wanafunzi kuwa watulivu.

“Ahadi zilizotolewa na serikali ni mbinu za kudumisha mfumo huu haramu ilhali tunaendelea kuteseka. Mfumo huo utaishia kuleta ubaguzi wa kielimu nchini badala ya usawa,” mwanafunzi mwingine wa chuo cha Moi alisema wakati wa maandamano hayo katika lango<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-5352755744671694"

     crossorigin="anonymous"></script>

Thursday 15 August 2024

MAMA TAIFA WA ZAMANI ZAMBIA MAUREEN MWANAWASA AAGA DUNIA NA MIAKA 61

 


ALIYEKUWA Mama wa Taifa nchini Zambia Maureen Mwanawasa amekufa akiwa na umri wa miaka 61.

Aliaga dunia Jumanne, Agosti 13, 2024, jioni akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Lusaka baada ya kuugua kwa muda mfupi, familia yake ilisema.

Bi Mwanawasa ni mkewe Rais wa tatu wa Zambia Levy Mwanawasa, aliyeongoza taifa hilo kuanzia mwaka wa 2002 hadi alipoaga dunia mnamo mwaka wa 2008.

Rais Hakainde Hichilema alituma risala za rambirambi akielezea kupokea habari za kifo cha Bi Mwanawasa “kwa mshtuko mkubwa.”

Kabla ya kifo cha mumewe mnamo 2008, Bi Mwanawasa alipigiwa upatu kurithi urais lakini baadaye aliamua kutowania wadhifa huo.

Mnamo mwaka wa 2016, mwendazake aliwania kiti cha Meya wa jiji la Lusaka lakini akabwagwa.

TRUMP AMPIGA KAMALA KWA MAMBO MAZITO HUKU UMAARUFU UKIENDELEA

 


MGOMBEAJI wa urais wa chama cha Republican, Donald Trump, Jumatano alishambulia sera za mpinzani wake wa chama cha Democratic, Kamala Harris, katika hotuba aliyotoa akiwa Asheville, North Carolina huku kura za maoni zikionyesha umaarufu wake unazidi kupungua.

Baadhi ya washirika, wafadhili, na washauri walionyesha wasiwasi kuhusu mashambulizi ya Trump kwa makamu huyo wa rais wa Amerika na kupendekeza alenge sera zilizofeli ambazo Harris alitetea akiwa afisini.

Akihutubia wafuasi wake, Trump aliepuka mashambulizi kuhusu rangi ya Harris na kuzamia sera zaidi kinyume na awali.

Lakini aliendelea kumtupia matusi ya kibinafsi, kwa kumuita mshenzi na kukejeli kicheko chake, akisema mpinzani wake ana shida kubwa.

Kujiondoa kwa Rais Joe Biden kwenye kinyang’anyiro cha urais Novemba 5 na kumuidhinisha Harris, mwezi uliopita, kulileta wimbi jipya katika kampeni.

Kura za maoni zinaonyesha Harris anaziba pengo la umaarufu dhidi ya Trump. Baadhi ya kura hizo zinaonyesha Harris yuko mbele katika kinyang’anyiro hicho cha Novemba 5.

Ujio wa Harris ulivuruga kampeni ya Trump, ambaye awali alitumia matusi huku akimlenga Makamu wa Rais ambaye mama yake alizaliwa India na baba yake Jamaica.

Trump alisema kuwa ataidhinisha hivyo basi kurahisisha mchakato wa kutoa vibali vya uchimbaji mafuta pamoja na kupunguza bei iwapo atamshinda Harris.

Pia aliahidi kupunguza bei za nishati na umeme kwa nusu, ndani ya miezi 12 hadi 18, baada ya kuingila mamlakani.

Hakubainisha wazi jinsi atakavyofanya hivyo, lakini alirudia ahadi za awali za kuongeza uzalishaji wa mafuta, ikiwemo katika Hifadhi ya Kitaifa ya Wanyamapori ya Artic, Alaska, ambapo utawala wa Biden ulisitisha utoaji wa vibali vipya.

Alimshutumu Harris kwa kuunga mkono marufuku ya kuchimba mafuta kwa kutumia teknolojia mwaka wa 2019 akisema msimamo wake utakuwa tatizo kubwa katika jimbo muhimu la Pennsylvania.

Kabla ya mkutano wa Trump huko Asheville, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampeni ya Harris, Michael Tyler, alituma taarifa akimshutumu Trump kwa kupuuza tabaka la kati kwa kupinga ulinzi wa vyama vya wafanyakazi na kuunga mkono kupunguzwa kwa ushuru wa makampuni.

Tyler alisema Harris atafanya ziara yake North Carolina, atakapozungumzia sera za kiuchumi katika hotuba yake huko Raleigh.

“Ataeleza mpango wa kupunguza gharama kwa familia za tabaka la kati na atakavyoshughulikia ushuru wa makampuni,” alisema Tyler.

Sunday 11 August 2024

HUENDA MATIANG'I AKAWA RAIS 2027 BAADA YA RUTO KUKOSA UMAARUFU

 

Aliyekuwa waziri zamani fred matiangi anayetaka urais
2027 

ULINGO wa siasa nchini huenda ukabadilika pakubwa iwapo aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani, Dkt Fred Matiang’i, atajibwaga katika kinyang’anyiro cha urais katika uchaguzi mkuu wa 2027.

Yamkini kutakuwa na mazingira mapya ya kisiasa iwapo Dkt Matiang’i atadumisha uungwaji mkono ambao vijana wanaashiria kumpa.

Duru zinasema kwamba Dkt Matiangi ameanza kujiandaa  kugombea urais kwa kuajiri kampuni ya kimataifa kusuka mikakati ya kufanikisha azma yake.

Wadadisi wa kisiasa wanasema kuna uwezekano atakuwa mwanasiasa anayemezewa mate na wagombeaji wengine wakitaka aungane nao.

Waziri huyo wa zamani anatambuliwa kwa misimamo yake mikali na maamuzi thabiti katika wizara tatu alizosimamia chini ya utawala wa Rais Uhuru Kenyatta.

 Japo amekuwa kimya, jina lake liliibuka katika kilele cha maandamano ya vijana kulalamikia gharama ya maisha na ufisadi serikali.

 Maandamano hayo yalipokuwa yakichacha, jina la Dkt Matiang’i,  ambaye  inasemekana anaishi ng’ambo liliibuka baadhi ya watumiaji wa mitandao wakimtaka  kujitokeza ili kujiunga nao kupigania uongozi bora na hata Rais wa Kenya 2027.

Vijana hao walisema kuwa Dkt Matiang’i alikuwa kiongozi aliyefanikiwa katika wizara mbalimbali alizosimamia.

“Matiang’i, mambo ni mawili: ujitokeze ama tuje tukuchukue. Tunahitaji uwe rais na si tafadhali,” Naomi Waithira aliandika kwenye mtandao wa X.

Kulingana na wadadisi wa kisiasa, iwapo umaarufu wake miongoni mwa vijana utadumu, Dkt Matiangi atakuwa mwanasiasa mwenye thamani kubwa katika uchaguzi mkuu ujao ikizingatiwa mikakati anayosemekana kutumia kujijenga na kujipigia debe.

 “Wanaofahamu mikakati ya siasa watakwambia kuwa jina la Dkt Matiang’i halikuibuka kwa bahati wakati  wa  kilele cha maandamano. Ni mkakati wa kutumia matukio yanayofuatiliwa na watu wengi kuwasilisha ujumbe ili ufikie watu wengi,” akasema mdadasi wa siasa Kephar Miruka.

“Akitumia mikakati kama hii bila kuchoka, na ikizingatiwa ushawishi na utendakazi  wake akiwa waziri ulioacha alama chanya  kwa Wakenya, basi atakuwa kama mwanamwali spesheli atakayewaniwa na wanasiasa wakitaka waungane naye katika uchaguzi mkuu wa 2027.”

Kulingana na mchambuzi huyu, Dkt Matiangi anaweza kunyima vigogo wa miaka mingi wa siasa kura za vijana kote nchini na za kaunti za Kisii na Nyamira na kuwa mfalme kivyake.

optimizelegibility; vertical-align: baseline;">Hii ni ikizingatiwa kuwa viongozi wa mashinani katika kaunti hizo  wanamuunga mkono.

Rais William Ruto atatetea kiti chake katika uchaguzi mkuu wa 2027.

Kufikia sasa, ni kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka ambaye ametangaza azma ya kumpinga Rais Ruto.

Kiongozi wa ODM Raila Odinga anagombea uenyekiti wa Tume ya Muungano wa Afrika ambao akishinda hataweza kugombea urais katika uchaguzi wa humu nchini.

Mwezi jana kakake, John Matiang’i alisema kuwa waziri huyo wa zamani  anafuatilia matukio ya siasa nchini.

 Bw  Miruka anasema  kwamba hata kabla ya maandamano ya vijana wa Gen Z dhidi ya serikali kuibuka, jina la Dkt Matiang’i lilikuwa vinywani mwa Wakenya.

“Anapendwa na Wakenya na zaidi ya yote na vijana ambao ndio idadi kubwa ya wapiga kura na wasio na ukabila. Hii pekee inakuonyesha kuwa ni mtu anayeungwa mkono na idadi kubwa ya wapiga kura na huyo ni mtu ambaye anaweza kuwatia tumbojoto wapinzani wake,” akasema.

Magavana Amos Nyaribo (Nyamira) na Simba Arati (Kisii), wamekuwa wakipigia debe kurejea kwa Dkt Matiang’i kwenye ulingo wa kisiasa.

“Tulikuwa na mtu wetu, Dkt Matiang’i, ninajua atakuja wakati unaofaa. Tutakuwa naye. Tuna viongozi wengine ambao watajibwaga uwanjani 2027. Tumedhamiria kuhakikisha kuwa siku moja, Omogusii (mtu wa jamii ya Abagusii) atakuwa kiongozi wa nchi,” akasema Bw Arati.

Wadadisi wanasema Matiang’i ana mtandao mkubwa wa marafiki aliounda akiwa waziri wa usalama wa ndani na ushirikishi wa serikali ya kitaifa ambao unaweza kufanya kupangua mikakati ya wagombeaji wengine wa urais katika uchaguzi mkuu wa 2027.

“Ninachojua ni kwamba atamezea mate sana na viongozi wengine na vyama vya kisiasa  wakitaka ndoa ya kisiasa,” akasema mchambuzi  wa siasa Dkt Isaac Gichuki.


KANISA KUFAIDI KWA KSHS.23MILIONI KWA KUUZIWA SHAMBA HEWA


 MAHAKAMA ya Mazingira na Ardhi imetoa uamuzi ambapo mwanamke mmoja anatakiwa kulipa kanisa la Katoliki Dayosisi ya Nakuru Sh23 Milioni.  

Sasa mwanamke huyo anatakiwa kurejesha pesa alizopokea kwa njia ya ulaghai baada ya kushtakiwa kwa kuuzia kanisa ardhi hewa.

Jaji Anthony Ombwayo alimwagiza Bi Hannah Wairimu Kahiga alipe pesa hizo zinazojumuisha Sh 19,800,000 ambazo kanisa lililipa kwa ununuzi wa shamba la ekari 11 katika eneo la Kiambogo, kaunti ndogo ya Naivasha na Sh 3, 960,000 kama fidia.

Uamuzi huo ulitolewa baada ya kubainika kuwa mshtakiwa aliuza shamba la mtu mwingine kwa kutumia hati bandia.

Bi Hannah Wairimu anadaiwa kushirikiana na maafisa katika afisi ya ardhi kuuza shamba hilo la ekari 11 ambalo ni sehemu ya shamba la Teresia Wanjiru Wangera aliyefariki 1981.

“Mshtakiwa wa Kwanza (Bi Wairimu) hajathibitisha kwa mahakama hii kwamba alipata hatimiliki kihalali na kiutaratibu alipouza mali hiyo kwa Mlalamishi (Kanisa Katoliki),” Jaji Ombwayo akaamua.

Kanisa kupitia wadhamini wake waliosajiliwa ambao maafisa wao wa sasa ni Maurice Muhatia, Askofu Mkuu Kisumu, baba Lawrence Mbogo na baba Simon Kamau walimwendea Bi Wairimu kwa nia ya kununua ardhi hiyo kwa mradi wa kanisa.

Thursday 8 August 2024

"WACHANA NA WAANDAMANAJI" AMERIKA YAONYA KENYA



 AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu.

Waziri msaidizi wa Usalama wa Raia, Demokrasia na Haki za Kibinadamu wa Amerika aliyezuru nchini Uzra Zeya ameelezea wasiwasi mkubwa wa nchi yake kuhusu ukatili wa polisi wa Kenya, akisema ni ukiukaji wa Katiba ya Kenya ya 2010.

Mwishoni mwa ziara yake ya siku mbili nchini Kenya, Bi Zeya ameitaka Kenya ijitolee kuzingatia sheria na kuheshimu haki za binadamu, kuchunguza visa vya kutoweka, utekaji nyara na kukamatwa kiholela kwa waandamanaji.

Akiwahutubia wanahabari katika Ubalozi wa Amerika kabla ya kuondoka nchini, Bi Zeya alifichua kwamba alisisitiza umuhimu wa uhuru wa kujieleza, kukusanyika na uhuru wa vyombo vya habari ili demokrasia iweze kustawi.  Bi Zeya aliyasisitiza haya alipokutana na Rais William Ruto, mashirika ya serikali na maafisa wakuu serikalini.

Shutuma dhidi ya makosa ya serikali kwa raia

“Katika mazungumzo yangu na Rais Ruto na maafisa wakuu wa Kenya, nilishutumu ghasia zilizofanywa dhidi ya waandamanaji waliodumisha amani, watetezi wa haki za binadamu na wanahabari na nikahimiza kulindwa kwa uhuru wa kimsingi wa kukusanyika kwa amani na kujieleza, kama ilivyo katika Katiba ya Kenya,” alisema.

“Pia nilisisitiza umuhimu mkubwa wa vikosi vya usalama kujizuia, kujiepusha na ghasia za aina zote, na uchunguzi wa haraka na uwajibikaji kwa matumizi ya nguvu kupita kiasi, na ukiukaji mwingine wa haki za binadamu uliotekelezwa na polisi.”

Alisema kuwa ziara yake nchini Kenya ilijiri wakati nchi inakabiliwa na wakati mgumu kwa demokrasia hasa katika kukabiliana na maandamano yanayoongozwa na vijana  wakitaka utawala bora na kulalamikia ufisadi.