HABARI KUU:

Mamia ya wanafunzi, wazazi, walimu na wahitimu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Peters Mwiruti katika Kaunti Ndogo ya Bumula, Kaunti ya Bungoma, walijaa katika uwanja wa shule kusherehekea baada ya kutangazwa kwa matokeo ya mtihani wa KCSE wa mwaka 2025, ambapo shule hiyo ilivunja rekodi yake ya awali ya kitaaluma..//..NAIROBI, KENYA, Alhamisi, Januari 1, 2026 – Kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM), Oburu Oginga, ametangaza wazi kuwa atakuwa mgombea wa urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2027 endapo ODM itaamua kugombea pekee bila kuingia muungano na vyama vingine..//..NAIROBI, KENYA, Jumanne, Januari 6, 2026 – Zaidi ya viongozi 42 wa matawi ya vyama vya wafanyakazi vilivyoambatanishwa na COTU-K wametangaza kumunga mkono mwenyekiti Francis Atwoli wakati anapojitayarisha kuwania muhula mwingine, utakaomfikisha zaidi ya miongo miwili madarakani.

Monday, 9 September 2024

MAANDAMANO YA WANAFUNZI KENYA

Mmoja wa wanafunzi wa somo la udaktari katika Chuo Kikuu cha Moi waliandamana mjini Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu, kupinga mfumo mpya wa ufadhili wa elimu ya chuo kikuu mnamo Septemba 9, 2024. PICHA | JARED NYATAYA

 WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Moi bewa kuu la  Kesses mjini Eldoret waliandamana Jumatatu wakitaka kufutiliwa mbali au kubadilishwa kwa mfumo mpya wa ufadhili wa masomo ya chuo kikuu.

Yalijiri licha ya viongozi wa kitaifa wa wanafunzi wa vyuo vikuu kupiga breki maandamano waliyopanga kufanya kote nchini kuanzia wiki hii, baada ya serikali kuahidi kwamba ungetathmini upya mfumo huo wa kufadhili elimu ya juu.

Hata hivyo, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Moi walishiriki maandamano kwa kuimba nyimbo za kupinga serikali na kubeba mabango yaliyopinga mtindo huo mpya wa ufadhili. Waliwataja viongozi wao wa kitaifa kama wasaliti.

 “Kama Chuo Kikuu cha Moi tunashikilia msimamo wetu kwamba tunakataa mtindo huu wa ufadhili. Siku 30 ambazo serikali imeomba ili kutathmini upya mfumo huo ni njama ya kutufumba macho hadi mwisho wa muhula wa sasa wa masomo,” alisema Enock Kwena mmoja  wa viongozi wa wanafunzi katika chuo hicho.

Wanafunzi hao walishutumu serikali kwa kutojali masaibu ya wanachuo.

Walisema hawana imani kamwe na utawala wa sasa na hususan ahadi iliyotolewa na Waziri wa Elimu Julius Ogamba; ya kuundwa kwa kamati mbili zitakazotathmini mfumo huo mpya wa ufadhili, akitoa wito kwa wanafunzi kuwa watulivu.

“Ahadi zilizotolewa na serikali ni mbinu za kudumisha mfumo huu haramu ilhali tunaendelea kuteseka. Mfumo huo utaishia kuleta ubaguzi wa kielimu nchini badala ya usawa,” mwanafunzi mwingine wa chuo cha Moi alisema wakati wa maandamano hayo katika lango<script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-5352755744671694"

     crossorigin="anonymous"></script>

No comments:

Post a Comment