HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Thursday 15 August 2024

MAMA TAIFA WA ZAMANI ZAMBIA MAUREEN MWANAWASA AAGA DUNIA NA MIAKA 61

 


ALIYEKUWA Mama wa Taifa nchini Zambia Maureen Mwanawasa amekufa akiwa na umri wa miaka 61.

Aliaga dunia Jumanne, Agosti 13, 2024, jioni akipokea matibabu katika hospitali moja jijini Lusaka baada ya kuugua kwa muda mfupi, familia yake ilisema.

Bi Mwanawasa ni mkewe Rais wa tatu wa Zambia Levy Mwanawasa, aliyeongoza taifa hilo kuanzia mwaka wa 2002 hadi alipoaga dunia mnamo mwaka wa 2008.

Rais Hakainde Hichilema alituma risala za rambirambi akielezea kupokea habari za kifo cha Bi Mwanawasa “kwa mshtuko mkubwa.”

Kabla ya kifo cha mumewe mnamo 2008, Bi Mwanawasa alipigiwa upatu kurithi urais lakini baadaye aliamua kutowania wadhifa huo.

Mnamo mwaka wa 2016, mwendazake aliwania kiti cha Meya wa jiji la Lusaka lakini akabwagwa.

No comments:

Post a Comment