HABARI KUU:

Mamia ya wanafunzi, wazazi, walimu na wahitimu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Peters Mwiruti katika Kaunti Ndogo ya Bumula, Kaunti ya Bungoma, walijaa katika uwanja wa shule kusherehekea baada ya kutangazwa kwa matokeo ya mtihani wa KCSE wa mwaka 2025, ambapo shule hiyo ilivunja rekodi yake ya awali ya kitaaluma..//..NAIROBI, KENYA, Alhamisi, Januari 1, 2026 – Kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM), Oburu Oginga, ametangaza wazi kuwa atakuwa mgombea wa urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2027 endapo ODM itaamua kugombea pekee bila kuingia muungano na vyama vingine..//..NAIROBI, KENYA, Jumanne, Januari 6, 2026 – Zaidi ya viongozi 42 wa matawi ya vyama vya wafanyakazi vilivyoambatanishwa na COTU-K wametangaza kumunga mkono mwenyekiti Francis Atwoli wakati anapojitayarisha kuwania muhula mwingine, utakaomfikisha zaidi ya miongo miwili madarakani.

Sunday, 15 September 2024

MOTO WATEKETEZA SHULE MACHAKOS JUMAPILI

MKASA wa moto umeripotiwa katika Shule ya Upili ya Katoloni iliyoko Kaunti ya Machakos. Kulingana na Shirika la Msalaba Mwekundu Nchini (KRC), moto huo ulitokea dakika chache baada ya saa tatu za usiku wa Jumamosi, Septemba 14, 2024. “Kisa cha moto kimeripotiwa katika Shule ya Upili ya Katoloni iliyoko Kaunti ya Machakos. Juhudi za kuuzima zinaendelea,” KRC ikasema kwenye ujumbe kupitia akaunti yake ya X. Hata hivyo, baadaye wafanyakazi wa shirika hilo la kushughulikia majanga wakishirikiana na wale wa Idara ya Zimamoto katika serikali ya Kaunti ya Machakos walifaulu kudhibiti na kuzima moto huo. “Shirika la Msalaba Mwekundu pia linatoa huduma ya kwanza katika eneo la tukio,” KRC iliandika kwenye X, baada ya muda wa saa tatu. Duru zinasema kuwa wanafunzi wawili walikimbizwa katika Hospitali ya Machakos Level 5, baada ya kuathiriwa na moshi uliotokana na moto huo. Visa kadhaa vya moto kuteketeza mali vimeripotiwa katika shule kadha nchini mwezi huu wa Septemba. Mkasa mbaya zaidi ulikuwa ni ule uliotokea usiku wa kuamkia Ijumaa, Septemba 6, 2024 Hillside Endarasha Academy, Nyeri ambapo jumla ya wanafunzi 17 walikufa papo hapo. Wengine wanne walikufa hospitalini kutokana na majeraha ya moto na hivyo kufikisha idadi jumla ya waliokufa kuwa 21.

No comments:

Post a Comment