HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Monday 16 September 2024

RAIS AKAIDI NA KUENDELEZA MICHANGO KANISANI HUKU AKITOA KSHS.1O MILION

 


RAIS William Ruto amefeli kudhihirisha kwa vitendo hatua yake ya kuzima maafisa wa serikali kushiriki michango ya harambee kama mojawapo ya njia za kupambana na ufisadi.

Alitoa agizo hilo Julai 2024 ili kuzima maandamano ya vijana wa Gen Z waliolalamika kuwa hulka ya viongozi na maafisa wakuu serikalini ya kutoa pesa nyingi katika michango hiyo inaendeleza uovu huo.

Wakati huo, Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi, ambaye ni mwandani wa Rais Ruto, alishutumiwa kwa kutoa Sh20 milioni, wakati mmoja, katika harambee, watu wakihoji asili ya pesa hizo.

Lakini Jumapili, Septemba 15, 2024, saa chache baada ya kuwasili nchini kutoka ziara rasmi nchini Ujerumani, Dkt Ruto pamoja na wandani wake walihudhuria Ibada katika Kanisa la Stewards Revival Pentecostal, Nairobi.

Wakati wa ibada hiyo, Rais alijitolea kusaidia katika ujenzi wa jengo jipya katika kanisa hilo baada ya jengo la zamani kubomolewa kutoa nafasi kwa upanuzi wa barabara ya Outering.

Aliahidi kutoa mchango wa Sh10 milioni kufadhili mradi huo licha ya kufahamu fika kuwa wananchi wanachukia mienendo ya viongozi kutoa michango ya aina hiyo, hali iliyolazimisha serikali kuidhibiti.

“Najulikana zaidi kama mshirika mkubwa katika miradi ya ujenzi wa makanisa. Unishirikishe hapo…….. Nimekubaliana na Askofu na nitatoa Sh10 milioni kufadhili ujenzi huu,” Rais Ruto akasema waumini wa kanisa hilo wakishangilia kwa furaha.

Hata hivyo, Rais alijaribu kufafanua kwamba kile alichofanya haikuwa harambee, bali ni “mchango tu”.

“Sharti tujenge kanisa hili kwa neema ya Mungu, tatakuja hapa kuizindua,’ akasema kiongozi wa nchi.

Alipokuwa akitangaza hatua ambazo serikali yake imeweka kuzuia maafisa wakuu na watumishi wa umma kushiriki michango ya harambee, Rais Ruto aliagiza Mwanasheria Mkuu kubuni sheria ya kufanikisha hatua hiyo.

No comments:

Post a Comment