HABARI KUU:

GACHAGUA ALIYEMUITA RAILA MAJINA SASA AMMEZEA MATE 2027..//..LUSAKA AMKAUKIA SENETA ONYONKA KWA KUMUITA MPUMBAVU!..//..GEN Z WA BANGALADESH WAVAMIA IKULU YA WAZIRI MKUU..//..AJALI SACHANGWAN HUKU WANAFUNZI 25 NA WAALIMU 3 WAKIPATA MAJERAHA MABAYA..//..MGOMBEA urais wa Chama cha Democrat Kamala Harris amemteua Gavana wa Minnesota Tim Walz kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi wa urais wa Novemba 5, mwaka huu.// AMERIKA imeonya serikali ya Kenya Kwanza dhidi ya kutumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji na kutaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu..//GAVANA wa Meru Kawira Mwangaza anataka Mahakama Kuu kuwahukumu maafisa wawili wa bunge la kaunti na MCA aliyeteuliwa kwa madai walidharau mahakama, akisema walipuuza maagizo ya korti kwa kukusudia kumtimua kwa mara ya tano.

Friday 19 July 2024

RAIS RUTO AKOSOLEWA KWENYE BARAZA LAKE JIPYA LA WATU 11 AKIWAHUSISHA WALIOFURUSHWA

Rais william ruto hatimaye ametangaza baraza la mawazi ambayo kwa sasa inakosolewa pakubwa na watu mbalimbali.je atayaweza Interior - Kithure Kindiki Health - Dr. Debra Mulongo Barasa Public Works - Alice Wahome Education - Julius Ogamba Defence - Aden Duale Agriculture - Dr. Andrew Karanja Environment - Soipan Tuya Water - Eric Muriithi Roads - Davis Chirchir ICT - Dr. Margaret Ndungu AG - Rebecca Miano

Wednesday 17 July 2024

KITUO CHA PEPEA RADIO SASA YASIKIKA VYEMA MTANDAONI

Sasa unawezasikiliza pepea radio inakuwa kivutio kikubwa kwenye mtandao kwa burudani tosha.bonyeza tu hii link hapa upate uhondo https://zeno.fm/radio/pepea-radio/ ama tafuta tu PEPEA RADIO kwenye google search

WANAHABARI WAPANGA MAANDAMANO TAREHE 24 JULAI

JUMATANO, Julai 24, 2024, itakuwa zamu ya wanahabari kujitokeza barabarani kote nchini kwa maandamano ya kupinga dhuluma wanazotendewa na polisi wakiwa kazini. Akitoa ilani kuhusu maandamano hayo, rais wa Chama cha Wahariri Nchini (KEG) Zubeida Kananu Jumatano alilaani visa vya wanahabari kushambuliwa na polisi wakiwa kazini akisema vinahujumu uhuru wao ambao unalindwa na katiba. Bi Kananu alitoa mifano ya visa vya hivi punde vya kupigwa risasi kwa ripota wa Shirika la Habari la Mediamax Catherine Wanjeri Kariuki na polisi wakikabiliana na waandamanaji mjini Nakuru na kutekwa nyara kwa mwanahabari mkongwe Macharia Gaitho na watu waliodaiwa kuwa maafisa wa polisi. “Kwa hivyo, tumekubaliana kwamba mnamo Jumatano wiki ijayo wanahabari watafanya maandamano kulaani vitendo kama hivi vya kikatili wanavyotendewa na polisi wanapotekeleza majukumu yao,” akasema alipoandamana na Bw Gaitho kuandikisha taarifa katika Afisi za Mamlaka ya Kuchunguza Utendakazi wa Polisi (IPOA). Hii ni kufuatia kisa cha Jumatano asubuhi ambapo mwanahabari huyo alitekwa mara na watu waliodai kuwa wao ni maafisa wa upelelezi kutoka Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI). Bw Gaitho alitendewa unyama huo katika Kituo cha Polisi cha Karen alikokimbilia baada ya kubaini kuwa alikuwa akiandamwa na maafisa hao waliokuwa kwenye gari la kibinafsi. Hata hivyo, baadaye DCI ilitoa taarifa ikidai maafisa wake walimkamata Bw Gaitho kimakosa kwani walikuwa wakimlenga mwanablogu Francis Gaitho. Bi Kananu alisema kuwa maandamano ya wanahabari yatakuwa ya amani na washiriki hawajihami kwa vitu vya kutishia amani. “Hatutajihami kwa mawe wala marungu, bali tutabeba kamera zetu, vijitabu na kalamu miongoni mwa vyombo vingine vya kazi. Sharti ulimwengu mzima ujue maovu yanayotendewa wanahabari nchini Kenya,” Bi Kananu akasema, akisisitiza. Katibu Mkuu wa Muungano wa Wanahabari Nchini (KUJ) Eric Oduor amethibitisha mipango ya maandamano hayo na kuwataka wanahabari wote nchini kushiriki. “Tutamjulisha rasmi Kaimu Inspekta Jenerali Douglas Kanja kuhusu nia yetu ya wanachama wetu kufanya maandamano kote nchini Jumatano wiki ijayo kupinga mwenendo wa polisi kushambulia wanachama wetu wakiwa kazini,” Bw Odour akaambia umma kwa njia ya simu.

SIMANZI KENYA JAJI OGEMBO AAGA DUNIA

Marehemu Jaji Daniel Ogembo, alipatikana Jumatano, Julai 17, 2024 akiwa ameaga dunia katika makazi yake rasmi mjini Siaya. Alitarajiwa kuongoza kikao asubuhi katika majengo ya Mahakama Kuu ya Siaya lakini akakosa kujitokeza hali iliyoibua shaka. Jaji Ogembo amehudumu kwa miaka miwili katika Mahakama Kuu ya Siaya alipokuwa jaji mkazi. Kamanda wa Polisi, Kaunti ya Siaya, Cleti Kimaiyo, alithibitisha kifo chake na kusema polisi na Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI) imeanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo. “Tutawafahamisha kuhusu matokeo, bado tunachunguza kiini cha kifo chake,” alisema mkuu wa polisi kaunti hiyo. Kulingana na afisa mmoja wa mahakama aliyechelea kutajwa kwa sababu ya uzito wa suala hilo, Jaji Ogembo alipatikana akiwa mfu asubuhi baada ya kukosa kujibu dereva wake alipokwenda kumchukua nyumbani kwake. “Dereva alimpeleka nyumbani Jumanne jioni lakini aliporejea asubuhi, jaji hakujibu hali iliyofanya dereva kuripoti kwa maafisa katika korti ya Siaya,” alisema afisa huyo wa ngazi ya juu. Kifo cha Jaji Ogembo kililemaza vikao vya korti huku wafanyakazi wakikumbwa na mshtuko kufuatia habari hizo. Kifo cha Jaji Ogembo kimetokea hata kabla ya wiki kuisha baada ya Jaji David Majanja kufariki dunia. Mwezi uliopita, Hakimu Mkuu wa Korti ya Makadara, Monicah Kivuti, aliuawa kwa kupigwa risasi na afisa mkuu wa polisi kutoka kituo cha Londiani.